Magonjwa
FAIDA ZA KUNYWA MAJI MENGI MWILINI
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2020/12/images-30.jpeg)
FAIDA ZA KUNYWA MAJI MENGI MWILINI
?Faida za Kunywa Maji mengi Mwilini Mfano;Wastani wa lita 2.5 kwa siku
- Kunywa Maji mengi hutibu tatizo la Kukosa Choo,pamoja na tatizo la kupata Choo kigumu
- Kunywa maji mengi husaidia kusafisha mwili na Kuondoa Sumu mwilini,hasa kwa Njia ya kukojoa
- Kunywa maji mengi husaidia kutibu magonjwa kama UTI(Urinary Track Infection) au kwa lugha ya Kiswahili ni maambukizi katika Njia ya Mkojo,ambapo tafiti zinaonyesha Unywaji wa maji Wastani wa lita 2.5 kwa siku,hupunguza uwezekano wa kupata UTI za mara kwa mara kwa zaidi ya asilimia 50%
- Unywaji wa maji mengi husaidia pia kutibu matatizo kama Kuumwa na KICHWA
- Kunywa maji mengi husaidia Ngozi ya mwili kunawiri kila wakati
- Unywaji Maji mengi husaidia kuzuia mtu kupatwa na Magonjwa Ya Moyo,Mfano; Utafiti uliofanyika Nchini Marekani kwa kipindi cha Miaka sita,husema kwamba unywaji waji Wastani wa Glasi 5 kila siku,husaidia kumkinga Mtu na magonjwa ya moyo kwa Wastani wa asilimi 41% zaidi ya wale wanaokunywa Glasi 2 au Chini ya hapa kwa siku
- Unywaji wa Maji mengi husaidia Kuupa Mwili Nguvu na kuondoa Uchovu kabsa.
- Kunywa Maji mengi husaidia kumkinga Mtu na Saratani ya Utumbo,kwani chakula na Usagaji wake utaenda vizuri kama Unakunywa Maji ya kutosha.
?Madhara ya Kutokunywa Maji mengi Mwilini
SUMMARY
Katika makala hii,tumegusia kuhusu Umuhim wa kunywa maji mengi mwilini,ambapo tumetaja baadhi ya Faida za Kunywa maji mengi mwilini,tukatolea Mfano wa wastani wa lita 2.5 Za Maji kwa siku
➖ KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584 PIGA SIMU AU TUMA UJUMBE,UTASIKILIZWA NA KUHUDUMIWA POPOTE ULIPO
#afya #Ushindi #Mtaji
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti1 day ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO
-
afyatips3 hours ago
Madhara ya damu kuwa nyingi mwilini