Ticker

6/recent/ticker-posts

MADHARA YA KUVAA VIATU VIREFU KWA WANAWAKE



  

 MADHARA YA KUVAA VIATU VIREFU KWA WANAWAKE

➡️ Ombeni Mkumbwa

➖SUMMARY

Wanawake wengi siku hizi huvaa viatu virefu kama Fashion.Japo tafti za kitaalam zinasema kuvaa viatu virefu kuna madhara yake Mengi tu;


Kuvaa Viatu Virefu kuna madhara Mengi ikiwemo;

✓Kupata maumivu ya Misuli ya Miguu,joint na mishipa ya damu kukaza

✓Kupata maumivu ya Mgongo na Kiuno

✓Kuwa katika hatari ya Kudondoka na kuleta madhara makubwa Mfano kwa Mjamzito

ℹ️MADHARA YA KUVAA VIATU VYENYE VISIGINO VIREFU AU VIATU VIREFU

(1) Maumivu ya mgongo

viatu virefu ni mtindo mpya au fashion kwa wadada wengi wa siku hizi wanaopenda mambo ya urembo, lakini pia hupendelewa sana na wasichana wafupi ili nao waonekane warefu.
kuna madhara mengi yatokanayo na uvaaji wa viatu hivi virefu na usipokua makini unaweza kudhani labda ni magonjwa mengine tu yanakuandama kumbe mchawi wako ni viatu vyako mwenyewe. hebu tuyaone madhara hayo kwa kirefu.
maumivu ya mgongo; katika hali ya kutembea na viatu virefu sana mtumiaji hukosa balance yaani uzito wa mwili wake unashindwa kubalance kati ya upande wa kushoto na kulia wa mwili wake hivyo hupata maumivu makali sana ya mgongo na kuhisi dalili za kutoneshwa akiguswa hasa sehemu za mgongo wa chini.

(2) Ugumba

Ugumba; kama nilivyosema kwenye pointi ya kwanza kukosa kwa balance ya mwili husababisha kupotea balance ya kwenye nyonga pia, hali hii hufanya mfuko wa uzazi kukaa vibaya na kua katika sehemu ambayo sio sahihi. hali hii huweza kumnyima mama mtoto na huambatana na dalili kama maumivu wakati wa tendo la ndoa, kushindwa kuzuia mkojo, na kushindwa kubeba mimba.

(3) Maumivu ya misuli ya nyuma ya miguu

maumivu ya misuli ya nyuma ya miguu; viatu virefu huleta maumivu makali ya nyama za nyuma ya mguu litaalamu kama calf muscles na ukiwachunguza vizuri watu wengi wanaovaa viatu hivyo hawawezi kusimama kwa muda mrefu yaani wataomba kiti wakae kila sehemu sababu ya maumivu makali, lakini pia mishipa huchomoza kwenye mishipa hiyo na kuleta maumivu inapoguswa.

(4) Kubadilika kwa muonekano wa Vidole

kubadilika kwa muonekano wa vidole; kutokana na kidole gumba kushindwa kuhimili mgandamizo unaopata kutoka kwenye mwili mzima, kidole hicho hujikuta kinapinda na kuleta shepu ambayo sio ya kawaida, hii sio nzuri sana kwa urembo na huweza kuleta maumivu.
mishipa ya damu kukunjika; mguu unaovishwa kiatu kirefu mara nyingi hujilazimisha kuingia kwenye kiatu kirefu na chembamba hii hufanya mishipa ya damu kujikunja sana na kua midogo sana na katika hali mbaya sana mishipa ya damu huweza kukatika.

(5) Maumivu ya joint ya mguu

maumivu ya joint ya mguu; presha kubwa kwenye joint ya mguu kitaalamu kama knee joint husababisha maumivu makali  ya joint hiyo na kua kama chanzo cha ugonjwa wa kuvimba na kuumwa joint kitaalamu kama osteoarthritis.

 (6) Kupinda kwa mgongo

kupinda kwa mgongo; kukosa kwa balance ya mwili wakati wa kutembea humfanya mtu kijaribu kupinda kidogo ili kupata balance, baada ya muda mrefu mgongo huanza kuzoea hali ile na kuleta maumivu makali yakiambatana na kupinda kwa eneo la juu na enoe la chini la mgongo.
 kuvunjika mifupa; baadhi ya watu wamewahi kupata ajali kwa kushindwa kuvihimili viatu virefu na kuanguka navyo, baadhi yao waliweza kuvunjika mifupa ya kisigino au mifupa ya vidole kama picha hapo chini inavyoonyesha.                          

(7) maumivu ya unyayo

katika matembezi ya kutumia viatu virefu kwa muda mrefu mgonjwa husikia maumivu makali ya kisigino, unyayo kwa chini na vidole kwa mbele, hii huweza kumnyima raha na kupunguza ufanisi wa shughuli zake za kila siku.

                               


KUMBUKA; JUKUMU LANGU KWAKO NI KUKUSHAURI,KUKUELIMISHA NA KUKUPA MSAADA WA KIAFYA PALE INAPOHITAJIKA.
    (Mawasiliano +255758286584 Tuma ujumbe utajibiwa kwa haraka zaidi)



Post a Comment

0 Comments