Magonjwa
TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)
TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)
SABABU ZA TATIZO HILI
Mvurugiko wa vichocheo mwilini (Hormonal imbalance) hausumbui wanawake tu kama tulivyozoea kusikia. Tatizo hili huweza kuwapata Na Wanaume pia
Tatizo hili huanza kuonekana kwa ukubwa wake kadri umri wa mwanamme unapozidi kuongezeka kwa kuwa vichocheo vya kiume (Testosterone) hupungua huku vile vya kike (Estrogen) vikianza kuongezeka. Ndipo hali hii husababisha baadhi ya tabia za kike kuonekana kwa mwanaume,Mfano mwanaume kuota matiti,kuwa na hips n.k
Kwa siku za hivi karibuni,mambo haya pia yameanza kutokea kwa vijana walio na umri mdogo
DALILI ZA TATIZO HILI La Matiti kwa Wanaume
-Mojawapo ya dalili za uwepo wa tatizo hili ni kuongezeka kwa ukubwa wa matiti ambayo wakati mwingine huanza hadi kutoa majimaji,
-uchovu usio na sababu maalumu,
-kuongezeka sana kwa uzito wa mwili (unene uliopitiliza)
-pamoja na kupungua sana kwa hamu ya tendo la ndoa au hata kushindwa kulishiriki kikamilifu.
Tatizo hili la Mwanaume kuota matiti(Gynecomastia) huhusisha kuongezeka kwa tishu ndani ya tezi za matiti ya Mwanaume, Na Uwiano usio sawa wa vichocheo(imbalance of the hormones) vya estrogen pamoja na testosterone ndyo sababu kubwa ya tatizo hili.
Tatizo hili la Gynecomastia linaweza kuathiri titi moja au yote mawili, na wakati mwingine ukubwa wa matiti hutofautiana kati ya titi moja na jingine hata kama yote yanaongezeka.
Kumbuka: Sio kila matiti yakiongezeka ni tatizo la Gynecomastia, Inaweza kuwa hali inayojulikana kama Pseudogynecomastia,
Pseudogynecomastia:
Hali hii huhusisha kuongezeka kwa mafuta na sio tishu ndani ya matiti ya Mwanaume.
Dalili za Tatizo la Matiti kuongezeka(Gynecomastia) ni pamoja na;
– Mwanaume kuanza kupata maumivu ya matiti
– Matiti kuanza kuongezeka ukubwa
– Kuhisi hali ya msisimko wa tofauti kwenye matiti baada ya kuyasugua,kugusa au kuguswa na nguo n.k
Hakikisha unapata Matibabu haraka ikiwa;
- Matiti yako yanavimba zaidi
- Unapata maumivu ya matiti
- Matiti yanaanza kutoa maji,usaha au damu
- Unahisi kitu kigumu kwenye titi au matiti
- Chuchu kuingia ndani
- Ngozi kujikunja Zaidi n.k
Sababu Zinazoongeza hatari Zaidi ya Mwanaume kuota Matiti
Hizi hapa ni baadhi ya Sababu zinazoongeza hatari Zaidi ya Mwanaume kupata tatizo hilo:
1. Mwanaume kufikia Umri wa balehe(Puberty).
2. Kuwa Mtu mzima Zaidi
3. Kuwa na tatizo la Uzito Mkubwa au Unene
4. Matumizi ya baadhi ya dawa jamii ya anabolic steroids hasa kwa Wanariadha
5. Kuwa na Matatizo mengine ya kiafya kama vile;
- Magonjwa ya Ini
- Magonjwa ya Figo
- Magonjwa ya Tezi la Thyroid
- Kuwa na Uvimbe(tumors)
- Au matatizo mengine kama vile, Klinefelter syndromen.k
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.