Connect with us

Magonjwa

UGONJWA WA SICKLE CELL(SELI MUNDU),NI NINI?,CHANZO CHAKE,DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE

Avatar photo

Published

on

UGONJWA WA SICKLE CELL(SELI MUNDU),NI NINI?,CHANZO CHAKE,DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE

         ?Yaliyomo Kwenye ukurasa huu;

  •  Utangulizi au Introduction
  • Chanzo cha tatizo la seli Mundu(sickle cell)
  • Dalili za uwepo wa seli mundu(sickle cell)
  • Vipimo vya Kufanya juu ya tatizo hili
  • Matibabu ya Tatizo la seli Mundu(Sickle cell)

UGONJWA WA SELIMUNDU AU SICKLE CELL

Ugonjwa wa seli mundu au kwa kitaalam hujulikana kama Sickle cell ni ugonjwa ambao hushambulia seli nyekundu za damu pamoja na Haemoglobin ambapo huhusisha kuishiwa kwa damu(anemia) kwa Mgonjwa hasa kutokana na seli nyekundu za damu kuwa shape au umbo lisilo la kawaida ambalo hupelekea seli hizo kufa mapema.

Hakuna tafiti zozote zinazoonyesha kwamba Selimundu Hushambulia Jinsia flani zaidi kuliko Nyingine.  Huku wagonjwa wengi zaidi wa tatizo hili wakipatikana afrika, ikifuatiwa na watu wa mashariki mwa Mediterania na Mashariki ya Kati. Kubadilika kwa seli nyekundu za damu na kuwa na shape isiyo yakawaida(Sickle shaped cells) husababisha mtu mwenye tatizo hili kuwa vigumu kuugua Ugonjwa wa malaria.  Inakadiriwa kuwa takriban 8% ya idadi ya watu wa Afrika ni homozygous kwa seli mundu (ambapo malaria imeenea zaidi).

 

 

 ? DALILI ZA UGONJWA WA SELI MUNDU-SICKLE CELL

Dalili za ugonjwa wa sickle cell kwa Ujumla zinahusisha zile zote za Mtu ambaye kaishiwa damu au ana ANEMIA kama vile;
 
– Kushindwa kupumua vizuri
 
– Kizunguzungu
 
– Maumivu ya kichwa
 
– Ubaridi katika viganja na miguuni
 
– Unjano katika macho na ngozi au jaundice
 
– Weupe katika viganja, na eneo la macho liitwalo conjuctiva, ulimi na midomo
 
– Maumivu ya tumbo
 
– Homa
 
– Maumivu ya viungo (joint pains)
 
– Maumivu ya kifua
 
– Damu katika mkojo (hematuria)

 – maumivu ya mfupa

 – kuziba kwa ateri kuu (CRAO)

– Vidonda vya miguu

 

 CHANZO CHA TATIZO LA SELI MUNDU-SICKLE CELL

 Ugonjwa hutokana na mabadiliko ya uorodheshaji wa jeni katika mnyororo wa beta ndani ya molekuli ya hemoglobini inayoitwa HbS.  Hasa, kuna uingizwaji wa glutamine kwa valine katika nafasi ya 6 katika mnyororo wa beta-globini.

 Neno “ugonjwa wa seli mundu” linatumika kwa wagonjwa wote ambao wana minyororo miwili isiyo ya kawaida ya beta.  Molekuli zinazosababisha hemoglobini huwa zinajikusanya pamoja kuwa polima ndefu, na kuifanya chembe nyekundu ya damu (RBC) kuinuliwa (umbo la mundu), kuwa ngumu na isiyoweza kuharibika ipasavyo wakati wa kupita kwenye sehemu ndogo na kusababisha kufungwa kwa mishipa.  RBC zisizo za kawaida pia huondolewa kutoka katika damu kwa kiwango cha kuongezeka, na kusababisha upungufu wa damu wa hemolytic 1.

 Watu walio na mnyororo mmoja wa beta ya HbS na mnyororo mmoja wa kawaida wa beta wanasemekana wana “tabia ya seli mundu”.  Kawaida hazina dalili, ingawa kuna uhusiano na hatari kubwa ya ugonjwa wa saratani ya figo. 2. Faida tu kwa watu walio na ugonjwa wa seli mundu ni kuongezeka kwa upinzani dhidi ya malaria.

 Watu walio na mnyororo mmoja wa beta ya HbS na mnyororo mmoja wa beta ya hemoglobin C (HbC), wana aina ndogo ya ugonjwa wa seli mundu inayojulikana kama ugonjwa wa hemoglobin SC (HbSC) 7.

?MATIBABU YA UGONJWA WA SELI MUNDU-SICKLE CELL

Matibabu ya ugonjwa wa seli Mundu au Sickle cell huhusisha sana hali ya mgonjwa. Lakini Kwa Ujumla,haya ndyo matibabu ya Seli Mundu.

➖ Kama mgonjwa atakuwa na matatizo katika mishipa yake midogo ya damu kitaalam tunaita Vaso-occlusive crisis, Lazima apewe maji kwa njia ya mishipa (dripu za normal saline na 5% dextrose), na pia dawa za kupunguza maumivu kama vile morphine, paracetamol au Diclofenac kulingana na atakavyoona mtaalam wa afya au daktari kuwa inafaa.

➖ Endapo mgonjwa atakuwa na matatizo ya ghafla katika kifua (acute chest syndrome) au matatizo ya kupungukiwa damu (aplastic crisis), anapaswa kuongezewa damu.

➖ Endapo mgonjwa atakuwa na  tatizo la acute chest syndrome au matatizo yeyote ya ugonjwa huu (any sickle cell crisis), atapaswa kupewa hewa ya oksijeni ili kuongeza kiwango cha hewa hiyo katika mzunguko wa damu.

➖ Lakini pia wagonjwa wote hupewa dawa za folic acid kwa ajili ya kuongeza damu, antibayotiki kwa ajili ya kupambana na maambukizi ya vimelea wa bacteria, na dawa za Hydroxyurea ambayo husaidia kupunguza kuvunjika vunjika kwa chembe nyekundu za damu.

➖ Kumbuka kwa sehemu zilizoendelea, watu wenye ugonjwa wa Seli Mundu hufanyiwa upandikizi wa supu ya mifupa kitaalam tunaita Bone marrow transplantation ambao umeonesha kuwa na manufaa makubwa hususani kwa watoto.

KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584

Karibu Sana..!!

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...