Magonjwa
FAHAMU KWA KINA TATIZO AU UGONJWA WA VITILIGO (UGONJWA UNAOIFANYA NGOZI KUPOTEZA RANGI YAKE)
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2021/01/IMG_20210625_081345_137.jpg)
FAHAMU KWA KINA TATIZO AU UGONJWA WA VITILIGO (UGONJWA UNAOIFANYA NGOZI KUPOTEZA RANGI YAKE)
• • • • • •
Ni tatizo linaloifanya ngozi ipoteze rangi yake ya asili. Sehemu zinazopoteza rangi huongezeka ukubwa kadri siku zinavyozidi kwenda. Tatizo hili linaweza kuathiri pia nywele,pamoja na sehemu ya ndani ya kinywa
Siku zote rangi ya ngozi na nywele za binadamu huamuliwa na vichocheo vya melanin. Vitiligo hutokea baada ya sehemu (seli) zinazozalisha vichocheo ya melanin kufa,au vikiacha kufanya kazi. Kwa msingi huu,kufa au kuacha kufanya kazi kwa seli zinazozalisha melanin kunaweza kusababishwa na mambo matatu
1.Matatizo kwenye mfumo wa ulinzi wa mwili ambao huanza kuzishambulia seli zake wenyewe kama maadui (wavamizi),jambo ambalo kitaalamu huitwa Autoimune condition
2.Kurithi
3.Mzio (allergy),stress pamoja na mionzi mikali ya jua au ajali kubwa ya ngozi
Tatizo hili siyo la kurogwa wala kuambukizwa,na haliwezi kumpata mtu mwingine kwa kugusana au hata kushirikiana naye mambo kadhaa kwenye jamii,hivyo tusiwatenge na kuwanyanyapaa wagonjwa wa tatizo hili ambao hupitia kipindi kigumu sana cha masongo wa mawazo,kuungua vikali na mwanga wa jua pamoja na matatizo ya kuona na kusikia
Tatizo hili halina tiba ya kudumu,hata hivyo msaada wa matibabu hutolewa kulingana na umri,ukubwa wa tatizo,jinsi maisha ya mtu yalivyo athirika pamoja na kasi ya kukua kwa tatizo.
Vyote hivi hulenga kuleta ahueni ya tatizo kwa mgonjwa pamoja na kuipunguza kasi ya kukua/kusambaa kwa tatizo hili.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Magonjwa6 days ago
Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu
-
magonjwa ya wanawake5 days ago
Dalili za Ectopic pregnancy,Mimba kutunga nje ya kizazi
-
Magonjwa2 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri4 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Events1 day ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
Uzazi/Ujauzito11 hours ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Events6 days ago
Princess Anne alilazwa hospitalini na majeraha madogo kufuatia tukio nyumbani kwake
-
News4 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI