Ticker

6/recent/ticker-posts

SIKU ZA HATARI YA KUPATA MIMBA(ovulation)



SIKU ZA HATARI

• • • • • •

SIKU ZA HATARI YA KUPATA MIMBA(ovulation)


Kipindi hiki ndipo yai huachiliwa kutoka kwenye mfuko wa yai(ovary),kipindi hiki hormone ya estrogen inayozalishwa hufanya tezi zilizoko kwenye uke kuzalisha ute mwingi kwa lengo la kusaidia mbegu za kiume zinapoingia ziweze kusafiri kwa urahisi kulifata yai lililoachiliwa.Ute huu unakua hauna rangi,mzito na unaovutika,uko kama ute wa yai bichi.


 KARIBIA NA HEDHI

Siku mbili au moja kabla ya kuanza bleed (Hedhi) wanawake hupata ute ambao unakua mzito kidogo na rangi yake inakua Inaelekea kuwa kama ya damu ya mzee(Brown), Siku unapoanza kupata kupata ute wa rangi hii ndo inakua siku ya kwanza kwenye mzunguko wako.

Hivyo unopata ute wenye rangi ya Brown siku unapokalibia siku za bleed ni kawaida. 


WAKATI WA UJAUZITO

Kipindi cha ujauzito pia hormone ya estrogen inazalishwa kwa wingi ili kuimarisha mji wa mimba,hormone hii inafanya tezi za kuta za uke kuzalisha ute ute mwingi.ute wa kipindi hiki unakua hauna rangi au unakua na rangi kama mawingu na hauna harufu kali.ute huu huzalishwa kwa wingi kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito 


WAKATI WA TENDO LA NDOA

Wakati wa ashiki ya tendo la ndoa uke huzalisha ute mwepesi ulio kama maji na unakua hauna harufu kali.


 WAKATI WA BAREHE

Kipindi binti anavunja ungo anapata ute mwingi,kutokana na kuongezeka kwa uzalishwaji wa hormone za uzazi hasa hormone ya estrogen. 


DAWA ZA UZAZI WA MPANGO

Pia matumizi ya dawa za uzazi wa mpango,hasa vidonge husababisha kuzalishwa kwa wingi ute.Ila unakua hauna rangi,harufu wala muwasho.


Bila shaka umeelewa jinsi gani ute wa kawaida unakuwa.Ute wowote unaoambatana na muwasho sehemu za siri na harufu kali ni dalili ya ugonjwa,upatapo hali hiyo vyema ukawahi hospitali ili kufanyiwa vipimo na kupata matibabu mapema.






Post a Comment

0 Comments