Magonjwa
UGONJWA WA RUBELLA KWA MJAMZITO
UGONJWA WA RUBELLA KWA MJAMZITO
Rubella ni ugonjwa wa kirusi unaosababishwa na kimelea aitwae rubella virus,Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya hewa ambapo mtu huambukizwa kwa kuvuta matone madogo madogo yatokayo kwa mtu mwenye ugonjwa huu (droplets infection) na matone haya huyapata kama mtu huyo akiwa anaongea,kukohoa au kupiga chafya karibu yako.
Maambukizi ya rubella hasa maambukizi mapya kwa mjamzito yanaweza kupelekea maambukizi ya mtoto aliepo tumboni (Congenital rubella Infectio (CRI)) ambayo yanaweza kuleta madhara makubwa sana kwa mimba na kiumbe kilichopo tumboni au mtoto akazaliwa akiwa na hitilafu mbalimbali katika mwili wake na za kudumu (Congenital Rubella syndromes (CRS)).
MADHARA YA RUBELLA KWA UJAUZITO
Sio wajawazito wote wenye rubella watakua na dalili au madhara makubwa ya kuonekana,walio wengi hawapati kashikashi yeyote na mimba inaweza kuenda vizuri tu na au baadae kupata mtoto mwenye tatizo au matatizo mbalimbali;mojawapo ya madhara ya ugonjwa huu kama yakitokea ni
1) Mimba kuharibika (miscarriages)
2) Kupata mtoto mfu (stillbirth)
MADHARA YA RUBELLA KWA MTOTO
1) Mtoto kudumaa tumboni (Fetal growth restriction)
2) Matatizo ya moyo kama matundu kwenye moyo nk (Cardiac defects)
3) Kua na ukungu ukungu kwenye macho (Cloudy cornea)
4) Mtoto wa jicho (cataract)
5) Presha ya macho ya watoto (infantile glaucoma)
6) Matatizo ya kusikia (Hearing loss)
7) Kuvimba ini na bandama (Hepatosplenomegaly)
8) Kuharisha harisha (diarrhea)
9) Manjano(jaundice)
10) Kutokwa na mitoki(Adenopathy)
11) Matatizo ya mapafu (Interstitial pneumonia)
12) Ngozi kua na vialama alama vyekundu au mabaka mabaka mekundu (Petechiae and purpura)
13) Wanakua na utosi wa mbele mkubwa kuliko kawaida (large anterior fontanelle)
14) Wanapata homa kali ya ubongo (Meningoencephalitis)
.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti22 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO