Magonjwa
UGONJWA WA UKOMA PAMOJA NA DALILI ZAKE
Dalili za UKOMA
……………
UGONJWA WA UKOMA PAMOJA NA DALILI ZAKE
Kwa kawaida Ugonjwa wa Ukoma ni ugonjwa ambao huathiri viungo mbali mbali vya mwili wa binadamu kama Vile Mikono,miguu,Macho,Uso pamoja na Ngozi pia.
UKOMA ni ugonjwa ambao huweza kuathiri viungo mbali mbali vya mwili,Na ugonjwa huu hujulikana pia kama Hansen’s disease au leprosy,
Kwa Mujibu wa Vituo vya Udhibiti na Kuzuia magonjwa yaani Centers for Diseases control and Prevention(CDC),
Ugonjwa huu husababishwa na bacteria ambao kasi yao ya Ukuaji ni ndogo sana(slow-growing bacteria), Na bacteria hawa Hujulikana kama Mycobacterium leprae.
Bacteria hawa huathiri mfumo wa fahamu au nerves, Ngozi,macho,pamoja na eneo la Puani kwenye nasal mucosa.
Ugonjwa huu ukigundulika Mapema na mgonjwa kupata Tiba,basi hupona kabsa,
WATU HUPATAJE UGONJWA WA UKOMA?
Haijulikani hasa jinsi ugonjwa wa Ukoma unavyoenea kati ya watu,
Ila Wanasayansi kwa sasa wanafikiri kuwa inaweza kutokea wakati mtu aliye na ugonjwa wa Ukoma anakohoa au kupiga chafya, na mtu ambaye hana kuvuta hewa ndani yenye matone yaliyo na bakteria hawa,
Hata hivo ni lazima kuwe na Ukaribu sana na wa muda mrefu na mtu aliye na ukoma ambao haujatibiwa kwa muda wa miezi mingi ili kupata ugonjwa huo,
Huwezi kupata ukoma unapomgusa mtu ambaye ana ugonjwa wa UKOMA au Kwa njia kama vile:
- Kupeana mikono
- kukumbatiana
- Kuketi karibu na mtu mwenye Ukoma kwenye basi
- Kuketi pamoja na mtu mwenye Ukoma wakati wa kula chakula n.k
Ugonjwa wa Ukoma pia hauambukizwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ambaye hajazaliwa wakati wa ujauzito na pia hauenezwi kwa njia ya kujamiiana.
Kutokana na hali ya ukuaji wa polepole wa bakteria na muda mrefu inachukua MUDA pia kuonekana kwa dalili za ugonjwa huo, na mara nyingi ni vigumu sana kupata chanzo cha maambukizi.
Pia Unaweza kuwa kwenye Hatari ya Kupata Ugonjwa wa Ukoma endapo unaishi kwenye maeneo au nchi ambapo Ugonjwa huu umesambaa Sana,
Kwa Mujibu wa Shirika la Afya Duniani(WHO)
Nchi ambazo ziliripoti Zaidi ya Cases Mpya 1,000 za Ugonjwa wa UKOMA( Hansen’s disease) kati ya Mwaka 2011 na 2015 ni Pamoja na:
(1) Africa:
- Democratic Republic of Congo
- Ethiopia
- Madagascar
- Mozambique
- Nigeria
- United Republic of Tanzania
(2) Asia:
- Bangladesh
- India
- Indonesia
- Myanmar
- Nepal
- Philippines
- Sri Lanka
(3) Americas:
- Brazil
BAADHI YA DALILI ZA UGONJWA WA UKOMA NI PAMOJA NA;
– Kukatika baadhi ya Viungo vya Mwili kama vile Vidole vya Miguu au mikono
– Ugonjwa wa ukoma huweza kusababisha Ganzi miguuni au mikononi pia
– Kuhisi hali ya kuchomwa eneo lote la Vidole vya miguuni au mikononi
– Vidole vya miguu pamoja na mikono kupooza
– Ugonjwa huu wa ukoma unaweza kusababisha matatizo ya macho ikiwa ni pamoja na upofu wa macho
– Ugonjwa huu wa ukoma huweza kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa shape ya Pua pamoja na Uso kwa Ujumla.
– Ugonjwa wa ukoma huweza kubadilisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa nyeusi na kuwa na vitu mithili ya ukurutu Hasa mikononi na miguuni.
MATIBABU YA UGONJWA WA UKOMA
Ugonjwa wa Ukoma hutibiwa kwa combination ya dawa mbali mbali Jamii ya antibiotics,
Na mara nyingi huhusisha Matumizi ya Dawa mbili au tatu(2/3) jamii ya antibiotics kwa Wakati Mmoja.
Na dawa hizo ni kama Vile; dapsone pamoja na rifampicin, na wakati mwingine mgonjwa huweza kuongezewa clofazimine kwa baadhi ya aina,
Aina hii ya Matibabu hujulikana kama multidrug therapy.
Njia hii ya matibabu husaidia kuzuia ongezeko la upinzani kwa antibiotic pamoja na bakteria wenyewe, ambayo inaweza kutokea kwa sababu ya matibabu haya kuchukua Muda mrefu zaidi.
Kwa kawaida Matibabu haya huweza kuchukua kati ya mwaka mmoja hadi miwili. Ugonjwa huo unaweza kuponywa ikiwa matibabu yatakamilika kama ilivyoagizwa.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LINALOKUSUMBUA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti23 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO