Magonjwa
UGONJWA WA VIKOPE(TRAKOMA),CHANZO,DALILI NA MATIBABU YAKE
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2021/02/images-13.jpeg)
UGONJWA WA VIKOPE(TRAKOMA),CHANZO,DALILI NA MATIBABU YAKE
Ugonjwa wa Vikope ambapo kwa kitaalam hujulikana kama TRAKOMA,ni ugonjwa ambao hutokea kwenye Kope za macho na kusababisha kope kujikunja kwa ndani hivo kuleta msuguano kati ya kope na kiyoo cha mbele cha jicho.
CHANZO CHA UGONJWA WA VIKOPE(TRAKOMA)
Ugonjwa wa Vikope au Trakoma husababishwa na Bacteria Jamii ya Klamidia Trakomati. Ambapo baada ya mgonjwa kushambuliwa na bacteria hawa matokeo yake ni kujikunja kwa kope kwa ndani nahivo kuleta hali ya msuguano mkubwa ndani ya jicho.
MADHARA YAKE;
– Mgonjwa kupata maumivu makali ndani ya jicho kwa sababu ya msuguano
– Jicho kubalika rangi na kuwa jekundu
– Mgonjwa kupata tatizo la uharibifu wa sehemu ya nje ya jicho yaani KONEA
– Lakini pia Mgonjwa anaweza kuwa Kipofu kabsa.
DALILI ZA UGONJWA WA VIKOPE(TRAKOMA)
• Mgonjwa kuwashwa na jicho lilioathirika
• Jicho kutoa machozi lenyewe
• Jicho kutoka uchafu kama matongotongo
• Rangi ya jicho kubalika na kuwa nyekundu
• Mgonjwa kupata maumivu makali ya jicho
• Kuwa na hali ya Msuguano ndani ya jicho
• Kope kuvimba na kujikunja kwa ndani,hivo sehemu ya ndani kuonekana kwa Nje.
MATIBABU YA UGONJWA WA VIKOPE(TRAKOMA)
Matibabu ya Ugonjwa wa Trakoma au Vikope ni pamoja na Matumizi ya Dawa kama Azthromycin na Tetracycline. Lakini ni vizur kwenda hospital kuchunguzwa kwanza kabla ya kutumia Dawa yoyote.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News5 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti1 day ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO