VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU KAMA UNA TATIZO LA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI

KUONGEZA WINGI WA DAMU

• • • • • •

VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU KAMA UNA TATIZO LA UPUNGUFU WA DAMU

Chembe hai nyekundu za damu maarufu kama Haemoglobin(hb) ndizo hutumika katika kuangalia kiwango cha Damu ambacho mtu anacho. 

Na kwa kutumia hizo ndyo tunaweza kusema mtu huyu ana damu nyingi au ana upungufu wa Damu mwilini.

Kiwango cha kawaida cha Damu kwenye mwili wa binadamu hutofautiana kati ya jinsia moja na nyingine, hapa namaanisha mwanamke na mwanaume katika kuangalia kiwango sahihi cha Damu ni tofauti kwa jinsia hizi mbili. 

Lakini pia ni tofauti kwa Mama Mjamzito kutokana na hatari ya kupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua.

✓ Mwanaume kiwango sahihi cha Damu ni g/dl 13.5 mpaka 17.5

✓ Kwa mwanamke ambaye si mjamzito,kiwango sahihi cha Damu ni g/dl 12.0 mpaka  15.5, hali hii ya kuwa na kiwango kidogo cha Damu ukilinganisha na mwanaume hutokana na mwanamke kupoteza damu kila anapoingia period au anapopata hedhi

✓ Na kwa mama Mjamzito,kiwango sahihi cha damu hutakiwa kuanzia g/dl 11 au 12 kwenda juu.

BAADHI YA SABABU ZA MTU KUWA NA UPUNGU WA DAMU MWILINI NI PAMOJA NA;

  • Ukosefu wa Madini ya Chuma mwilini
  • Ukosefu wa Vitamin mwilini  hasa hasa Vitamin B12
  • Upungufu wa damu mwilini kwa sababu ya magonjwa kama Kansa, Magonjwa ya Figo na Ukimwi
  • Upungufu wa damu mwilini kutokana na ugonjwa wa MALARIA
  • Upungufu wa damu mwilini kutokana na hali ya damu kushindwa kuganda kwa kitaalam huitwa Coagulopathy
  • Matumizi ya baadhi ya dawa,Sumu,makemiko au magonjwa ambayo huathiri utengenezaji wa Seli nyekundu za Damu(Red blood cells)
  • Tatizo la selimundu au Sickle cell anemia
  • N.K
BAADHI YA VYAKULA VYA KUONGEZA DAMU MWILINI NI PAMOJA NA;

1. Baadhi ya matunda husaidia kwa kiwango kikubwa katika kuongeza damu mwilini, na matunda hayo ni pamoja na; Matunda Damu, Zabibu, machungwa, maembe,nyanya pamoja na Strawberries.

2. Ulaji wa mbogamboga kama vile matembele,Spinach au Sukuma wiki pia husaidia kwa kiwango kikubwa kuongeza damu. Pendelea kula mboga mboga hasa hasa mboga jamii ya matembele zitakusaidia sana kuongeza wingi wa damu mwilini.

3. Pendelea kula vyakula vywenye vyanzo vizuri vya Madini aina ya Chuma Kama vile; maharage,nyama au maini.

4. Matumizi ya juisi mbali mbali kama juisi ya Rozella,BeetRoot,Tikiti maji, karoti au nyanya huongeza Damu kwa kasi sana. Hivo pendelea kutumia aina hizi za Juisi.

5. Zipo njia nyingine za kuongeza Damu katika mwili wa Binadamu kama vile; matumizi ya Dawa aina ya FEFOL ambapo hapa kuna kiwango kikubwa cha madini ya chuma ambayo yatasaidia utengenezwaji wa haraka wa damu,na hivo kuongeza kiwango cha damu mwilini.

Endapo Mgonjwa yupo katika hali ya hatari ya kuishiwa na damu,zipo njia za haraka kama kutundikiwa damu moja kwa moja kwa njia ya Drip.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comments

WEKA COMMENT HAPA..!!!