Connect with us

new

CHANZO CHA TATIZO LA KUPATWA NA KIUNGULIA(Au kwa kitaalam heartburn)

Published

on

 KIUNGULIA

• • • • •

CHANZO CHA TATIZO LA KUPATWA NA KIUNGULIA(Au kwa kitaalam heartburn)


Tatizo hili huwapata watu wengi, wakiwemo wakina mama wajawazito.  Zipo sababu kadhaa ambazo huchangia mtu kupatwa na hali ya kiungulia,na miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na;


–  Kwa mama mjamzito, Mabadiliko ya vichocheo mwilini ambayo hutokea kipindi cha mimba,ndyo husababisha hali ya kiungulia. Hapa nazumgumzia vichocheo vya Progestrone pamoja na Relaxin


(i). Uzalishwaji mkubwa wa Kichocheo cha Progestrone kwenye damu kipindi cha ujauzito husababisha chakula kitembee taratibu pamoja na mmeng’enyo wake kwenda taratibu sana.


(ii). Uzalishwaji mkubwa wa kichocheo cha Relaxin kwenye damu kipindi cha ujauzito husababisha njia ya chakula yaani Oesophagus kutanuka, pamoja ma vichikizoo vya tumbo kulegea yaani Sphinter hali ambayo hupelekea chakula kilichopo tumboni kilichochanganyika na Acid kupanda juu, Hali hii husababisha kiungulia kikali kwa mama mjamzito


– Kula kwa wingi vyakula vyenye acid kali kama Maharage,kula vyakula vya mafuta mengi, Nyanya N.K


– Kunywa pombe kupita kiasi

N.K


DALILI ZA KIUNGULIA NI PAMOJA NA;


– Kuhisi hali ya kuchomwa inayopanda kifuani


– Kuhisi ladha ya kitu kichungu Mdomoni


– Na mara chache maumivu wakati wa kumeza mate


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

afya

Sababu za Mimba Kutunga Nje ya Kizazi pamoja na Dalili zake(Ectopic pregnancy)

Published

on

   AFYA YA UZAZI

• • • •

Sababu za Mimba Kutunga Nje ya Kizazi pamoja na Dalili zake(Ectopic pregnancy)


 Kwa asilimia kubwa Mimba kutunga Nje ya kizazi yaani kwa kitaalam Ectopic pregnancy hutokea wakati yai lililorutubishwa kukwama ndani ya mirija ya uzazi(fallopian tubes) au kuelekea kwenye  njia ya uzazi, japo mimba kutunga sehemu nyingine yoyote mbali na sehemu yake ya kawaida ndani ya kizazi bado ni Ectopic pregnancy,


CHANZO CHA TATIZO HILI LA MIMBA KUTUNGA NJE YA KIZAZI


– mara nyingi mimba hutunga nje ya kizazi kwa sababu mirija ya uzazi yaani fallopian tubes imeharibiwa, kuziba au kufungwa vibaya. 


– Tatizo la mvurugiko wa vichocheo mwilini(hormone imbalance) au ukuaji usiokuwa wa kawaida wa yai lililorutubishwa pia linaweza kuchangia tatizo hili.



• Vitu vingine ambavyo vinaweza kuchangia tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi ni pamoja na:


 ✓ Kuwa na tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi kwenye ujauzito wa nyuma. Ikiwa umewahi kuwa na ujauzito wa aina hii hapo awali, una uwezekano mkubwa wa kuwa na mwingine.


✓ Uvimbe au maambukizi ya magonjwa mbali mbali.  Maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama; kisonono au chlamydia, yanaweza kusababisha kuvimba kwenye mirija na viungo vingine vya karibu, na kuongeza hatari ya ujauzito kutunga nje ya kizazi(ectopic pregnancy).


✓ Matibabu kwa ajili ya kupata mtoto.  Utafiti mwingine unaonyesha kwamba wanawake ambao wamewahi kufanyiwa In- Vitro fertilization (IVF) kwa ajili ya kupata watoto au matibabu kama hayo wana uwezekano wa kuwa na tatizo la ujauzito kutunga nje ya kizazi(ectopic pregnancy). 


Pia kukaa kwa muda mrefu sana bila kuzaa au kuzaa mapema sana huweza kuongeza uwezakano wa tatizo


 ✓ Upasuaji katika mirija ya uzazi(Tubal surgery).  Upasuaji wa kurekebisha tatizo lolote kwenye mirija ya uzazi yaani fallopian tubes huongeza hatari ya Mwanamke kupatwa na tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi.


 ✓ Aina ya njia ya uzazi wa mpango ulioichagua.  Uwezekano wa kupata ujauzito wakati unatumia kifaa kama intrauterine device (IUD) ni mdogo sana. 


Lakini endapo kwa bahati mbaya ikitokea umebeba mimba na una kifaa cha IUD ndani yako, uwezekano wa mimba kutunga nje ya kizazi ni mkubwa.


  Njia ya kufunga uzazi(Tubal ligation), njia hii ni ya kudumu ya kudhibiti uzazi lakini ikiwa utapata ujauzito baada ya utaratibu huu uwezekano wa mimba hyo kutunga nje ya kizazi ni asilimia 100.


✓ Uvutaji sigara.  Uvutaji sigara kabla tu ya kupata ujauzito unaweza kuongeza hatari ya ujauzito kutunga nje ya kizazi.  Kadri unavyovuta sigara, ndivyo hatari inavyo kuwa kubwa zaidi.


DALILI ZA MIMBA KUTUNGA NJE YA KIZAZI


 Huenda usione dalili yoyote mwanzoni. wanawake wengi ambao wana tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi(ectopic pregnancy) wanapata dalili zote za awali za ujauzito  kama vile; kukosa period au kutokuona siku zao za hedhi, matiti kujaa, kichefuchefu N.k.


 Ikiwa unapima ujauzito au mimba, matokeo yatakuwa mazuri tu kama kawaida na kuonyesha kwamba wewe ni mjamzito.  Tofauti tu ni kwamba matatizo huanza kutokea pale ujauzito unavyozidi kukua.


 – Mara nyingi, dalili za kwanza kabsa kama una tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi ni damu nyepesi kuanza kutoka ukeni na maumivu ya kiuno au nyonga.


 Ikiwa damu huvuja kutoka kwenye mirija ya uzazi(fallopian tubes), unaweza kuhisi maumivu ya bega au hamu ya kuwa na haja kubwa.  Dalili maalum hutegemea mahali damu inajikusanya na mishipa ipi inaathiriwa.


 Ikiwa yai lililorutubishwa linaendelea kukua kwenye mrija wa fallopian, linaweza kusababisha mrija huo wa uzazi kupasuka.  Matokeo yake ni Kutokwa na damu nzito ndani ya tumbo la uzazi.  Dalili  kama hii huweza kuhatarisha maisha,kusababisha maumivu makali ya kichwa, kuzimia na mshtuko.


 KUMBUKA; NENDA HOSPITAL HARAKA UKIONA DALILI KAMA HIZI HAPA;


 • Maumivu makali ya tumbo na kutokwa na damu ukeni


 • Maumivu makali ya Kichwa au kuzimia


 • Maumivu ya bega N.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Continue Reading

afya

DALILI 8 AMBAZO MTU HUWEZA KUZIPATA BAADA YA KIDONDA CHAKE KUSHAMBULIWA NA BACTERIA

Published

on

DALILI 8 AMBAZO MTU HUWEZA KUZIPATA BAADA YA KIDONDA CHAKE KUSHAMBULIWA NA BACTERIA


1. Homa

 Baada ya upasuaji, ni kawaida kwa wagonjwa kuwa na homa kwa kiwango cha chini ya digrii 100 Fahrenheit. lakini, ikiwa joto la mwili lipo juu hadi 101 au zaidi, hiyo inaweza kuonyesha uwezekano wa maambukizi ya vimelea vya magonjwa kama vile Bacteria katika kidonda. 

 Wagonjwa ambao wana homa wanaweza pia kuwa na tatizo la maumivu ya kichwa na kupungua kwa hamu ya kula.

Vidonda vilivyoshambiwa na Bacteria vinaweza kupatiwa tiba ya antimicrobial drugs n.k.

 2. Mwili kuchoka kupita kiasi

 Kumuuliza mgonjwa jinsi anavyohisi inaweza kusaidia kutathmini uwepo wa maambukizi katika kidonda.

Kupata uchovu wa mwili kupita kiasi pamoja na mwili kukosa nguvu huweza kuwa kiashiria mojawapo cha uwepo wa maambukizi kwenye kidonda au jeraha ulilonalo.

 3. Kidonda kutoa usaha au maji maji yenye rangi ya Kijani au Njano

 Katika hali ya kawaida kidonda kinatakiwa kiwe na rangi nyekundu, hii ndyo ishara nzuri ya kidonda kuelekea kupona kwa urahisi

 4. Kuongezeka kwa Maumivu katika Jeraha au Kidonda

 Kwa ujumla, mgonjwa anayeendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji au  kuwa na jeraha/kidonda anapaswa kuona unafuu na maumivu yanayopungua na sio kuongezeka.  

Ikiwa mgonjwa ana maumivu yanayoongezeka badala kupungua, hiyo inaweza kuwa dalili ya maambukizi katika jeraha au kidonda. 

 5.Uwekundu Kuzunguka Jeraha au kidonda huku ndani ya kidonda kukiwa na rangi ya tofauti kama vile njano au kijani

 Hapo awali, vidonda vinaonekana vyekundu kidogo kwa sababu ya mchakato wa uchochezi wa asili wa uponyaji, lakini uwekundu huo unapaswa kupungua polepole kwa takribani siku 5-7. 

 Uwekundu zaidi karibu na jeraha huku ndani ya kidonda kukiwa na rangi nyingine ya tofauti kama njano au kijani ni ishara ya maambukizi katika jeraha. 

 6. Uvimbe wa Eneo Lililojeruhiwa

 Kama uwekundu, uvimbe ni kawaida katika hatua za mwanzo za uponyaji wa jeraha. lakini, uvimbe unapaswa kupungua kila wakati.  Uvimbe wa kudumu inaweza kuwa ishara ya maambukizi au shida zingine kwenye kidonda.

 7. Joto La Ngozi Inayozunguka kidonda

 Ingawa inaweza kuwa kawaida kwa ngozi inayozunguka jeraha kuhisi joto kali, Lakini endapo ngozi inayozunguka kidonda huhisi joto sana kwa kugusa bila kupoa, hiyo inaweza kuonyesha kwamba mwili unapanga mashambulizi dhidi ya maambukizi. 

 Joto husababishwa na kutolewa kwa kemikali za vasoactive zinazoongeza mtiririko wa damu kwenye eneo hilo.  Kwa kuongezea, mfumo wa kinga hutoa joto zaidi kwa kutuma lymphocyte kutoa kingamwili kuharibu pathogen na phagocytes kumeza bakteria waliokufa.

 8. Kupoteza uwezo wa kufanya kazi katika kiungo chenye jeraha au kidonda

 Ishara nyingine ya maambukizi kwenye jeraha ambayo inaweza kuhitaji matibabu, ni wakati mgonjwa amepoteza uwezo wa kiutendaji kwenye kiungo au eneo lilithoathiriwa. 

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Continue Reading

afya

Dalili za Tetanus(pepopunda)baada ya mtu kuchomwa na kitu chenye Ncha kali

Published

on

TETANUS

• • • • • •

 Dalili za Tetanus(pepopunda) baada ya mtu kuchomwa na kitu chenye Ncha kali


Tetanus ni ugonjwa  hatari sana ambao kwa kiswahili hujulikana kama Pepopunda,Ugonjwa huu huhusisha athari kwenye mfumo wa Fahamu inayosababishwa na sumu ya Bacteria(toxin-producing bacterium)


Sumu hii kutoka kwa Bacteria mtu huweza kuipata baada ya kuchomwa na vitu vya ncha kali kama vile Misumari,Mabati,Chupa,sindano n.k


DALILI ZA TETANUS AU PEPOPUNDA


 -Wastani kutoka kuambukizwa hadi kuonekana kwa ishara na dalili (kipindi cha incubation) ni siku 10.  Kipindi cha incubation kinaweza kuchukua siku 3 hadi 21.


 Ishara na dalili za tetanus au pepopunda huanza pole pole kisha huendelea kuwa mbaya zaidi ndani ya wiki mbili.  Kawaida dalili huanza kuonekana kwenye taya na kuendelea kushuka chini ya mwilini.


 Ishara na dalili za pepopunda ni pamoja na:


1. Misuli ya mwili kuwa na maumivu makali na kuwa migumu au kukakamaa,ugumu wa misuli kwenye taya n.k


 2. Mvutano wa misuli kuzunguka midomo yako, wakati mwingine hutengeneza  kitu kinaitwa persistent grin


3.Misuli kukamaa na kuparalize au kupooza katika maeneo ya shingoni

 

4. Kupata shida sana ya kumeza kitu


 5. Misuli ya tumboni kuwa migumu sana


 6. Kukua kwa ugonjwa wa pepopunda husababisha maumivu yanayojirudia, pamoja na mgonjwa kupata mshtuko ambao hudumu kwa dakika kadhaa (spasms). 


7. Kwa Kawaida, shingo na upande wa nyuma pamoja na miguu huwa migumu, mikono hunyooka kwa mbele huku ngumi zimekunjwa. 


8. Ugumu wa misuli kwenye shingo na tumbo unaweza kusababisha shida ya kupumua.



 • Kadri ugonjwa unavyoendelea, ishara zingine na dalili zinaweza kuonekana kama vile;


 1. Shinikizo la damu kuwa juu au Mtu kuwa na Presha ya kupanda(High blood pressure)


 2. Mapigo ya moyo kwenda mbio sana


3. Joto la mwili kuwa juu sana au mtu kuwa na Homa kali


 4. Mgonjwa kuvuja Jasho sana mwilini

N.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




Continue Reading

Trending

Copyright © 2017 Zox News Theme. Theme by MVP Themes, powered by WordPress.