Connect with us

Magonjwa

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

Avatar photo

Published

on

 UGONJWA WA KISONONO

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa ambao husababishwa na Bacteria ambaye kwa kitaalam hujulikana kama Neisseria gonorrhoeae na kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana.

Ugonjwa huu wa zinaa hushambulia na kuathiri zaidi maeneo ya mwili yenye joto Pamoja na Unyevu unyevu kama vile;

  •  Kwenye urethra au mrija ambao huvuta mkojo kutoka kwenye kibofu
  • Kwenye macho
  •  Eneo la Kooni
  • Ukeni
  • kwenye Uume
  •  Kwenye njia ya haja kubwa(anus)
  • Kwenye Via vya Uzazi vya Mwanamke ikiwemo Kwenye Kizazi,Mirija ya Uzazi, Pamoja na Mlango wa kizazi yaani cervix n.k

UGONJWA WA KISONONO HUSAMBAAJE AU KUAMBUKIZWA?

Ugonjwa huu husambazwa kwa Njia ya Kujamiiana,

Kufanya Mapenzi kwa njia ya Mdomo,Sehemu ya haja kubwa au Ukeni yaani oral, anal, or vaginal sex.

Kutumia kondomu au njia nyingine ya kizuizi unaposhiriki tendo la ndoa kunaweza kusaidia sana kupunguza uwezekano wako wa kusambaza au kuambukizwa magonjwa ya zinaa kama vile kisonono,

Kumbuka tu matumizi ya njia hizi hayataondoa kabisa hatari ya wewe kupata magonjwa kama haya, hasa ikiwa hutumii kwa Usahihi,

Unaweza kutumia Njia kama Condom na bado ukapata Kisonono(Gono) endapo hukutumia kwa Usahihi wake.

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO);

Kumbuka; Ugonjwa huu wa kisonono kwa asilimia kubwa ni vigumu mwanamke kuonyesha dalili za moja kwa moja hata kama ameambukizwa. Lakini kama akionyesha dalili basi baadhi ya dalili kama hizi hapa chini huweza kutokea.

MIONGONI MWA DALILI AMBAZO HUWEZA KUJIONYESHA KWA MWANAMKE NI PAMOJA NA;

– Mwanamke kupatwa na tatizo la maumivu makali wakati wa kufanya mapenzi

– Mwanamke kutokwa na maji maji ukeni ambayo yana harufu sana

– Mwanamke kutokwa na ute ute ambayo umechanganyika na usaha ukeni

– Kutokwa na damu baada ya kufanya tendo la ndoa

– Kupatwa na shida ya blid mara mbili ndani ya mwezi mmoja

– Kupatwa na maumivu makali ya tumbo

– Joto la mwili kupanda au kuwa na homa

– Kuvimba kwenye eneo la mashavu ya uke 

DALILI ZA UGONJWA WA KISONONO KWA MWANAUME NI PAMOJA NA;

– Kutokwa na usaha sehemu za Siri

– Kuwashwa kwenye kitundu ambacho mkojo hupita

– Kupatwa na hali ya kuchomwa wakati wa kukojoa ambayo tunasema kwa kitaalam burning sensation

– Mwanaume kupatwa na tatizo la kushindwa kukojoa kabsa au mkojo kugoma kutoka, kitu ambacho huweza kumsababishia maumivu makali pamoja na mahangaiko

– Kukojoa mkojo ambao umechanganyika na Damu

– Joto la mwili kupanda au kuwa na homa

MADHARA YA UGONJWA WA KISONONO

je kisonono kinaweza kusababisha matatizo gani?

(1) Ikiwa wewe ni Mwanamke, una nafasi kubwa ya kukumbwa na matatizo ya muda mrefu kutokana na ugonjwa wa kisonono kama hukupata Tiba ukapona,

Magonjwa ya zinaa yasiyotibiwa kama vile kisonono na Chlamydia yanaweza kuleta athari kwenye njia ya uzazi na kuathiri maeneo mbali mbali ikiwemo Kizazi chenyewe(Uterus), mirija ya uzazi Pamoja na ovaries.

Hii inaweza kusababisha matatizo mengine kama vile maambukizi ya bacteria kwenye via vya Uzazi vya Mwanamke yaani pelvic inflammatory (PID),

PID inaweza kusababisha maumivu makali, ya muda mrefu na uharibifu wa viungo vya uzazi.

– Kuziba au kupata kovu kwenye mirija ya uzazi,

Na hii huweza kuleta madhara mengine kama vile;

  • kufanya iwe vigumu zaidi Kwa mwanamke kupata mimba
  • kusababisha tatizo la mimba kutunga nje ya Kizazi yaani ectopic pregnancy,
  • Kisonono kinaweza pia kusababisha shida ya mtoto kuzaliwa kabla ya wakati wa kujifungua(Njiti/premature)

(2) Ikiwa wewe ni Mwanaume,Kisonono kinaweza kusababisha:

  • kovu kwenye urethra
  •  Kupata jipu ndani ya uume wako, ambalo linaweza kuathiri uwezo wako wa kutungisha Mimba
  • Kupata tatizo la Epididymitis, au kuvimba kwa mirija ya kubebea shahawa karibu na korodani zako
  • Maambukizi ambayo hayajatibiwa yanaweza pia kuenea kwenye mfumo wako wa damu, ambapo yanaweza kusababisha matatizo adimu kutokea lakini makubwa kama vile ugonjwa wa baridi yabisi(arthritis) pamoja na uharibifu wa valve ndani ya moyo.

MATIBABU YA UGONJWA WA KISONONO

Ni vizuri kwenda hospital kufanyiwa vipimo kwanza kabla ya dawa, Na baada ya hapo kama utagundulika una tatizo hili basi utapata matibabu sahihi kulingana na ugonjwa wako pamoja na hatua ulipofikia.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa4 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...