Connect with us

afyatips

MATUMIZI YA DAWA ZA ASILI KUONGEZA UCHUNGU KWA MJAMZITO(madhara yake)

Doctor Ombeni

Published

on

Imeboreshwa July 10, 2026 by Doctor Ombeni

  UJAUZITO

• • • • •

MATUMIZI YA DAWA ZA ASILI KUONGEZA UCHUNGU KWA MJAMZITO(madhara yake)


Zipo imani nyingi na zipo tamaduni mbali mbali za baadhi ya watu, kuhusu matumizi ya dawa za asili kwenye kuongeza uchungu kwa mama mjamzito.


Huku wengine wakiwa na imani kwamba mama mjamzito akitumia dawa hizo hujifungua kwa haraka zaidi.


Dawa hizo hutumiwa kwa njia mbali mbali huku zingine zikifichwa katika sehemu za siri za mwanamke,eti kwa lengo la kuongeza uchungu kwa mama huyu.


Je nini madhara yake?


Kuna vitu vingi vya kitaalam lazima uvifahamu kwa mama mjamzito kabla ya kufanya kitu chochote.


Vit hivo ni pamoja na hali ya mtoto aliyetumboni, mlalo wake, historia ya mama kwa mimba za nyuma, hali ya kondo la nyuma au placenta ikoje N.K


Endapo umetumia dawa hizo za asili kwa ajili ya kuongeza uchangu wakati mama ana matatizo mengine nini kitatokea?


Mfano; Huwezi ukamuongezea uchangu wa mama kujifungua kawaida wakati kondo lake la nyuma limeziba kabsa njia ya mtoto kupita, 


huwezi kumuongezea mama uchungu wa kuzaa kawaida wakati ana kovu au kidonda kikubwa cha operation za mimba za nyuma, matokeo yake ni kusababisha mtoto kufia tumboni,mtoto kuzaliwa na ulemavu, mama kupasuka kizazi,mama kufariki N.K


Na kwa bahati mbaya,asilimia kubwa ya watu ambao wanatumia dawa hizi,hata huo uchungu hauongezeki bali hata kusukuma tu mtoto wanashindwa.


KUMBUKA;Epuka matumizi ya dawa hovio kwa ajili ya afya yako na afya ya mtoto aliyetumboni.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



🏆Certified| Doctor from Afyaclass.Hapa utapata Ushauri & Tiba juu ya magonjwa mbali mbali. Kwa msaada Zaidi Tuwasiliane kupitia namba: +255758286584.Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.