Ticker

6/recent/ticker-posts

MWANAMKE KUPATA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA( Tatizo kwa Wanawake wengi)



 MAUMIVU

• • • • • •

MWANAMKE KUPATA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA( Tatizo kwa Wanawake wengi)



Wanawake wengi wanalalamika juu ya tatizo hili pasipo kujua sababu hasa ya shida hii ni ipi.

Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuchangia mwanamke kupata maumivu makali wakati wa tendo la Ndoa.


SABABU ZA MWANAMKE KUPATA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA NI PAMOJA NA;


- Hali ya ukavu ukeni ambayo huweza kusababisha hali ya  msuguano mkali,michubuko, na vidonda, mwisho wa siku mwanamke hupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.


- Maambukizi ya magonjwa mbali mbali kama vile UTI,FANGASI pamoja na maambukizi katika via vya uzazi vya mwanamke yaani PID


- Tatizo la mvurugiko wa vichocheo mwilini yaani Hormone imbalance. Fahamu kwamba katika sehemu za siri za Mwanamke kuna Tezi ambalo hufanya kazi ya kuzalisha maji maji,uteute na kuleta hali ya unyevu na ulaini ukeni,kwani sehemu za siri za mwanamke katika hali ya kawaida hazitakiwi kuwa kavu. Hivo basi mabadiliko ya vichocheo mwilini huweza kuathiri utendaji kazi wa tezi hili,kwani linafanya kazi chini ya udhibiti wa vichocheo vya mwili au hormones.


- Matumizi ya baadhi ya kemikali wakati wa kuoga na wakati wa tendo la ndoa. Baadhi ya kemikali ambapo zingine zipo kwenye sabuni za kuogea huweza kusababisha hali ya mabadiliko makubwa ya mazingira ya ukeni,ikiwa ni pamoja na kuleta hali ya ukavu pamoja na maumivu makali wakati wa tendo la Ndoa.


Habari njema ni kwamba tatizo hili linatibika na kuisha kabsa.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments