Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA APPENDIX AU KIDOLE TUMBO(chanzo,dalili na tiba yake)



  APPENDIX

• • • •

UGONJWA WA APPENDIX AU KIDOLE TUMBO(chanzo,dalili na tiba yake)


Kwa kawaida,appendix au kidole tumbo ni sehemu ya muendelezo wa utumbo mkubwa au mpana mwishoni, ambapo huwa na kitu mithili ya kidole chako cha mwisho cha mkononi.


CHANZO CHA TATIZO LA APPENDIX


Kwa kawaida baada ya chakula kuyeyushwa na umeng'enyaji kuendelea, kuna baadhi ya myeyusho wa chakula hupitia sehemu hii ya kidole tumbo au appendix.


Sasa endapo chakula kitapita hapa pamoja na vitu vidogo vidogo vigumu kama vile; mchanga N.K, vitu hivi haviwezi kupita hapa, hivo hujilundika hapa kila siku unapokula chakula kilichochanganyika na vitu hivi vigumu. 


Hali hii huendelea hadi kufikia hatua ya kidole tumbo au appendix kuziba kwa juu pamoja na kuvimba na mtu kuanza kupata maumivu makali. Hapo ndipo chanzo cha tatizo la appendix huanza.


DALILI ZA UGONJWA WA APPENDIX AU KIDOLE TUMBO NI PAMOJA NA;


- Kupatwa na maumivu makali ya tumbo usawa wa kitovu chako kuelekea upande wa kulia


- Joto la mwili kupanda au kuanza kuwa na homa


- Kupatwa na hali ya kichefu chefu pamoja na kutapika


- Mgonjwa kupatwa na shida ya tumbo kujaa gesi mara kwa mara

N.K


VIPIMO


vipo baadhi ya vipimo ambavyo huweza kufanyika kama vipimo vya damu,ultrasound,Ct Scan N.K


Mgonjwa anaweza kuchunguzwa dalili,historia ya ugonjwa pamoja na uchunguzi kwa njia ya kupapasa mikono ambayo hufanywa na mtaalam wa afya au dactari.



MATIBABU YA UGONJWA WA APPENDIX


- Matibabu ya ugonjwa wa kidole tumbo au appendix huhusisha matumizi ya dawa mbali mbali katika hatua za mwanzoni za ugonjwa, lakini kama tatizo litaendelea mgonjwa atafanyiwa upasuaji na kuondoa kabsa hicho kidole tumbo.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments