Connect with us

magonjwa ya watoto

Chanzo Cha Tatizo La Mtoto kutoa Matongotongo machoni pamoja na Tiba yake

Doctor Ombeni

Published

on

530 Views
2 Comments

MATONGOTONGO MACHONI

CHANZO CHA TATIZO LA MTOTO KUTOA MATONGOTONGO MACHONI PAMOJA NA TIBA YAKE

Tatizo hili huweza kumpata mtoto mara tu baada ya kuzaliwa na kadri anavyokuwa pia huweza kupata shida hii.

Hivo basi hakuna mda maalum au umri maalum wa kupatwa na shida hii, Mtoto mwenye umri wowote huweza kupatwa na shida hii ya macho kutoa matongotongo yenyewe.

Kitaalam ni kwamba endapo macho yatatoa matongo tongo yenyewe, basi hiyo ni ishara kwamba kuna kitu hakiko sawa ndani ya jicho lako, au kwa lugha nyingine kuna tatizo katika jicho lako.

CHANZO CHA TATIZO LA MTOTO KUTOA MATONGOTONGO MACHONI NI PAMOJA NA;

1. Ishara ya maambukizi ya magonjwa ya zinaaa kutoka kwa mama,Mfano; kaswende na kisonono

2. Mtoto kupatwa na ugonjwa wowote wa macho mfano; ugonjwa wa vikope(Trakoma) Ambapo kope huvimba na kujikunja kwa kuingia ndani hivo cha ndani kuonekana kwa nje

3. Sababu zingine ni jicho kuumia kutokana na vitu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuanguka na kugongwa sehemu ya jicho

4. Kitu chochote ambacho hakitakiwi kuingia ndani ya jicho,Mfano mchanga N.K

5. Jicho kuumia kwa kuchomwa na vitu vya Ncha kali

6. Kuingiwa na sumu au makemikali mbali mbali Kwenye Jicho ikiwemo ya Dawa za mimea N.K

DALILI ZA MACHO KUTOA MATONGOTONGO NI PAMOJA NA;

– Macho kuanza kuwasha mara kwa mara licha ya kupikicha na kusugua macho

– Macho kuanza kubadilika rangi na kuwa manjano au mekundu

– Maumivu ya macho

– Macho kuanza kutoa machozi yenyewe

– Macho kuanza kutoa matongotongo kila wakati licha ya kusafishwa vizuri

MATIBABU YA MACHO KUTOA MATONGOTONGO

Matibabu ya tatizo hili la macho ya mtoto kutoa matongotongo hutegemea chanzo chake, uchunguzi wa kina huhitajika kwa mtoto, ila dawa mbali mbali huweza kutumika hilo tatizo likaisha.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Utokaji wa uchafu kwenye macho kwa kawaida hauna madhara na wakati mwingine huisha wenyewe.  Hata hivyo, kutokwa na uchafu unaotokea pamoja na dalili nyingine katika eneo la jicho, kama vile Jicho kuvimba,kupata maumivu makali n.k kunaweza kuonyesha maambukizi au tatizo lingine la jicho.  Mzazi au mlezi wa mtoto mchanga aliye na dalili hizi atahitaji kushauriana na daktari.

Makala hii inazungumzia jinsi kutokwa na tongotongo kwenye macho ya mtoto huweza kuwa na athari,na inaelezea jinsi ya kutibu shida hii.  Pia inazungumzia, sababu nyingine, matatizo yanayoweza kutokea na wakati wa kuwasiliana na daktari.

 Kutokwa na maji au tongotongo kwenye macho kwa sababu ya mfereji wa machozi ulioziba ni kawaida kwa watoto wachanga, Hali hii  Inathiri angalau asilimia 6% ya watoto wachanga.

 Katika baadhi ya matukio, kutokwa na damu kwenye macho kunaweza kutokea. Ikiwa ni hivyo, matibabu ya haraka yanaweza kuhitajika.

Daktari anaweza kusaidia kuamua sababu ya kutokwa kwa jicho, na kushauri juu ya matibabu yoyote muhimu au tiba za nyumbani ambazo zinaweza kusaidia.
Sababu ya kawaida ya kutokwa na Uchafu au matongotongo kwenye macho ni Mrija au duct iliyoziba ya machozi,Kulingana na Hospitali ya Watoto ya Boston, angalau asilimia 6% ya watoto wachanga wana mfereji wa machozi ulioziba.  Hali hii inaweza kutokea kwa sababu mwisho wa mfereji wa machozi haufunguki vizuri wakati mtoto anazaliwa.
Machozi huundwa kwenye tezi ya macho, ambayo inakaa juu ya jicho.  Maji ya machozi husaidia kusafisha na kulainisha sehemu ya jicho.  Wakati mtu anapepesa macho, kope hufagia maji ya machozi kwenye mifereji hii, ambayo huimwaga ndani ya pua.
Ikiwa kitu kitazuia mirija ya machozi, Maji yanaweza kukosa tena sehemu ya kutoka kwenye uso wa jicho.  Vizuizi vinaweza kusababisha macho kuwa na maji sana, kutokwa na uchafu au matongotongo.n.k

Conjunctivitis;

Kutokwa na Uchafu au matongotongo kwenye macho ya watoto wachanga inaweza kuwa ishara ya ugonjwa au matatizo kama vile conjunctivitis, au pinkeye.
Conjunctivitis ni kuvimba kwa conjunctiva, utando mwembamba unaolinda sehemu ya mbele ya jicho.
 Tofauti na njia ya machozi iliyoziba, conjunctivitis mara nyingi husababisha sehemu nyeupe ya jicho kuonekana nyekundu.
Kulingana na aina ya maambukizi kwenye conjunctiva, dalili kwa kawaida huonekana ndani ya siku 1 hadi 12,baada ya mtoto kuzaliwa.

Dalili za conjunctivitis kwa watoto wachanga zinaweza kujumuisha:

 – Macho kutoa matongotongo,machozi au kutokwa na uchafu mwingine kwenye macho

– kope za macho kuvimba au kuwa laini, na mara nyingi zinaweza kubadilika rangi kwenye ngozi yake

– Macho kuwa mekundu,n.k

Tatizo la Conjunctivitis kwa watoto wachanga wakati mwingine linaweza kutokea kando ya njia ya machozi iliyoziba.  Hata hivyo, mjamzito anaweza pia kumwambukiza mtoto wake maambukizi ya bakteria au virusi wakati wa kujifungua, na hivyo kusababisha tatizo la conjunctivitis.

Kuwashwa kutokana na kemikali;

Kuwashwa kwa sababu ya kemikali kuingia machoni kunaweza pia kusababisha kuvimba kwa conjanctiva kwa watoto wachanga.

Wataalamu wa matibabu wanaweza kuwapa watoto wachanga dawa ya macho ndani ya saa 2 hadi 3 baada ya kuzaliwa ili kuzuia maambukizi.  Matone haya ya jicho wakati mwingine yanaweza kusababisha hali ya kukereketa na kuwasha ambayo inaweza kusababisha dalili za conjunctivitis.

Tatizo la Conjunctivitis kutokana na athari ya kemikali kwa watoto wachanga kawaida huchukua masaa 24 hadi 36.

Matibabu ya nyumbani kwa tatizo la kutokwa na Matongotongo machoni;

  • Ikiwa kutokwa na matongotomgo jichoni kunatokana na njia ya machozi iliyoziba, kwa kawaida huisha yenyewe wakati mtoto anakaribia umri wa mwaka 1.
  • Hata hivyo, upepo, hali ya hewa ya baridi, na mwangaza mkali wa jua pia vinaweza kuzidisha dalili, kwa hivyo mzazi au mlezi anapaswa kulinda macho ya mtoto mchanga kutokana na vitu hivi.

Kusafisha Uchafu Machoni;

Mzazi au mlezi mara nyingi anaweza kumtibu mtoto mchanga na kuzibua tundu la machozi lililoziba hata akiwa nyumbani.  Kabla ya kugusa eneo la karibu na macho ya mtoto, ni muhimu kuosha mikono kwa sabuni na maji ya joto ili kuzuia maambukizi.  Mtu anapaswa pia kutunza, kuosha mikono vizuri baada ya kuisafisha ili kuzuia kupaka sabuni kwenye jicho la mtoto.

 Ili kuondoa usaha au matongotongo, chovya pamba safi au kitambaa laini kwenye maji ya uvuguvugu, kisha uifute
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

References:

  1. . HealthyChildren.org – Pinkeye (Conjunctivitis). Inaelezea sababu, dalili na matibabu ya matongotongo machoni kwa watoto.
  2. . Conjunctivitis (Pink Eye). Mwongozo kuhusu aina za conjunctivitis, jinsi ya kuzuia na matibabu.
  3. . Primary Eye Care / Eye Health. Hutoa miongozo kuhusu afya ya macho na maambukizi ya macho kwa watoto.
  4. . Sura kuhusu magonjwa ya macho kwa watoto, ikijumuisha conjunctivitis na neonatal eye infections.
  5. . Rejea ya kitabibu kuhusu utambuzi na usimamizi wa magonjwa mbalimbali ya macho.

530 Views
2 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

2 Comments

2 Comments

  1. Guest Avatar

    Rehema Kibona

    September 3, 2026 at 6:43 am

    Asante sana kwa kunifungua macho Mtaalam.

    • Doctor Ombeni

      Doctor Ombeni

      September 3, 2026 at 6:46 am

      Asante sana

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

magonjwa1 year ago

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba Genital warts ni ugonjwa gani,Soma Zaidi hapa kufahamu Genital warts ni moja ya aina...

magonjwa2 years ago

Vipele Sehemu Ya Siri,Vipele Ukeni, Vipele Kwenye Uume

VIPELE SEHEMU YA SIRI,VIPELE UKENI, VIPELE KWENYE UUME Vipele kwenye Uume: Vipele Kwenye Uume: Chanzo, Dalili na Matibabu Tatizo la...

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips1 day ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti1 day ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

531
2