Ticker

6/recent/ticker-posts

JE INACHUKUA MUDA GANI UGONJWA WA UKIMWI KUANZA KUONYESHA DALILI?



 UKIMWI

• • • • •

JE INACHUKUA MUDA GANI UGONJWA WA UKIMWI KUANZA KUONYESHA DALILI?


Hapa tunazungumzia baada ya mtu kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi itachukua muda gani kuanza kupata dalili za ugonjwa huu wa ukimwi,


Hili ni swali ambalo watu wengi hujiuliza na wanapenda kujua,hivi baada ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi dalili huchukua muda gani kuanza kuonekana.


MAJIBU; Dalili za awali kabsa  baada ya mtu kuambukizwa virusi vya ukimwi huanza kuonekana baada ya Wiki 2 mpaka 4, na mara nyingi dalili hizo ni kama vile;


✓ Mtu kuanza kupata homa za mara kwa mara


✓ Mtu kupata maumivu makali ya misuli ya mwili


✓ Mtu kuanza kuvimba tezi mbali mbali za mwili wake kama vile; tezi za shingoni n.k


✓ Mtu kuanza kupata rashes kwenye ngozi


✓ Mtu kuhisi baridi kali mwilini pasipo kujua chanzo (chills)


✓ Mwili kuchoka kupita kawaida


✓ Kuhisi hali ya madonda kooni, na wengine ngozi ya ndani ya mdomo kwa juu huanza kuona hali ya kubabuka au vidonda vidonda


✓ Kupata maumivu makali ya kichwa mara kwa mara

n.k


Kwa baadhi ya watu ugonjwa huu wa ukimwi hauonyeshi dalili kabsa ukiwa katika hatua za mwanzoni


- Baadae mtu huanza kupata dalili mbali mbali kama vile;


• Kuanza kukohoa sana


• Kupata shida sana ya upumuaji


• Uzito wa mwili kushuka kwa kasi na mtu kuanza kukonda sana


• Kupatwa na homa kali


• Mtu kuchoka sana kupita kawaida


• Kuharisha sana mara kwa mara

n.k


🔻 SUMMARY;


- Dalili za mwanzo au awali za maambukizi ya virusi vya ukimwi huweza kuonekana baada ya wiki 2-4 


- Sio kila mtu huweza kuonyesha dalili hizi za awali kwenye kipindi hiki


- Asilimia 98% ya maambukizi ya Virusi vya ukimwi huchukua kipindi cha Miezi 3 toka siku ya kuambukizwa, ili kuonekana kwenye kipimo cha ukimwi


- Rudia kupima baada ya miezi 3 kupata majibu sahihi


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments