Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA MVURUGIKO WA TUMBO(chanzo,dalili na tiba)



 TUMBO

• • • • •

TATIZO LA MVURUGIKO WA TUMBO(chanzo,dalili na tiba)


✓ Tatizo la mvurugiko wa tumbo ni tatizo ambalo huhusisha dalili mbali mbali kama vile;


- Tumbo kunguruma sana


- Mtu kupata maumivu ya tumbo


- Mtu kuharisha mara kwa mara


- Mtu kutoa harufu mbaya(kujamba) mara kwa mara


- Na wakati mwingine mtu kupata kichefuchefu pamoja na kutapika


CHANZO CHA TATIZO LA MVURUGIKO WA TUMBO


- Zipo sababu mbalimbali za mtu kupatwa na shida ya mvurugiko wa tumbo, na baadhi ya sababu hizo ni kama vile;


• Kula vyakula ambavyo vinauchafu ndani yake


• Kunywa maji ambayo sio masafi,mfano maji yalichonganyika na vinyesi au uchafu mwingine


• Kula kitu chenye kemikali flani au sumu


• Kula vyakula ambazo vinasababisha gesi kwa kiwango kikubwa


• Kula mchanganyiko wa vyakula vingi, kwa kiasi kikubwa na kwa wakati mmoja


• Mashambulizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa kama vile; Bacteria, Minyoo,amiba n.k


MATIBABU YA TATIZO HILI LA MVURUGIKO WA TUMBO


- Tatizo hili huweza kutibiwa kulingana na chanzo cha tatizo, Japo huweza kuhusisha matumizi ya dawa mbali mbali kama vile; Metronidazole au Flagyl n.k


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments