Ticker

6/recent/ticker-posts

CHANJO ZA MTOTO TOKA ANAZALIWA MPAKA ANAPOFIKIA UMRI WA MIAKA 5



  CHANJO ZA MTOTO

• • • • •

CHANJO ZA MTOTO TOKA ANAZALIWA MPAKA ANAPOFIKIA UMRI WA MIAKA 5


1. Chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Kifua Kikuu Maarufu kama BCG


chanjo hii hutolewa kwa njia ya sindano bega la kulia, na huchomwa mara tu baada ya mtoto kuzaliwa au mara ya kwanza anapofika kliniki kama hakupewa baada ya kuzaliwa,


Endapo KOVU halijatokea Begani, chanjo hii hurudiwa baada ya miezi 3


2. Chanjo ya Kuzuia ugonjwa wa Kupooza Yaani POLIO


Chanjo hii hutolewa kwa njia ya matone mdomoni mara tu baada ya mtoto kuzaliwa au mara ya kwanza anapofika kliniki kama hakupewa baada ya kuzaliwa,


Halafu hurudiwa baada ya mwezi 1, 2, na 3.


3. Chanjo ya PENTAVALENT(DTP)


chanjo hii huzuia magonjwa matano yaani; Donda koo,kifaduro,pepopunda,homa ya ini, na homa ya manjano


chanjo hii hutolewa kwa njia ya sindano ya paja la Kushoto na hutolewa mtoto akiwa na umri wa mwezi 1, hurudiwa mwezi 2 na 3.


4. Chanjo ya PCV13


Chanjo hii husaidia kuzuia ugonjwa wa Pneumonia kwa mtoto


chanjo hii hutolewa kwa njia ya sindano ya paja la Kulia na hutolewa mtoto akiwa na umri wa mwezi 1, hurudiwa mwezi 2 na 3.


5. Chanjo ya ROTAX


chanjo hii ni kwa ajili ya kuzuia ugonjwa wa Kuharisha kwa mtoto,


na hutolewa mtoto akiwa na umri wa mwezi 1 na kurudiwa mwezi 2.


6. Chanjo ya kuzuia ugonjwa wa SURUA


Chanjo hii hutolewa mtoto akiwa na umri wa miezi 9 na miezi 18


7. VITAMIN A


Mtoto hupata vitamin A supplements akiwa na umri wa kuanzia miezi 6, 12,18,24,30,36,42 na 54


8. Dawa za MINYOO


Dawa za minyoo huanza kutolewa mtoto akiwa na umri wa kuanzia miezi 12,18,24,30,36,42 na 54



kwa Maelezo Zaidi na Msaada kuhusu kusoma KADI yako Ya KLINIKI Bofya hapa..!!


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments