Ticker

6/recent/ticker-posts

KUPEVUSHWA KWA YAI/MAYAI au Ovulation(Kwa Wanawake)



 OVULATION

• • • • •

KUPEVUSHWA KWA YAI au Ovulation(Kwa Wanawake)


Kupevushwa kwa yai, ni pale ambapo yai hutoka kwenye vifuko vya mayai yaani Ovaries na kuingia kwenye mirija ya uzazi ambayo hujulikana kwa kitaalam kama fallopian tubes, kitendo hiki ndyo kinaitwa OVULATION.


FAHAMU BAADHI YA MAMBO KUHUSU UPEVUSHAJI WA MAYAI AU OVULATION


1. Upevushaji wa mayai huhusiana na yai kutoka kwenye vifuko(ovaries) vyake kwenda kwenye mirija ya uzazi


2. Upevushaji wa mayai au Ovulation hutokea siku ya 14 kwa Wanawake wenye mzunguko wa siku 28


3. Ili mwanamke apate mimba lazima upevushaji wa mayai utokee


4. Kuna baadhi ya wanawake wenye matatizo ya mayai kutokupevushwa kabsa au kutokupevushwa kwa wakati


5. Mwanamke huweza kupevusha mayai mawili kwa wakati mmoja yaani kutoka ovary ya kulia na kushoto japo ni mara chache kutokea, hapa ndipo mapacha wasio Fanana huweza kupatikana yaani Fraternal twins baada ya urutubishaji wa mayai yote mawili


6. Baada ya mayai kutoka kwenye vifuko vyake(ovaries) huingia kwenye mirija ya uzazi yaani fallopian tubes, Na endapo mwanamke akafanya mapenzi na mwanaume kipindi hiki huweza kupata ujauzito


7. Kama urutubishaji wa yai umeshatokea,moja kwa moja kiumbe huenda kujishikiza kwenye kuta za mji wa mimba kitendo ambacho hujulikana kama Implantation na kuendelea kukua mpaka mtoto azaliwe,


Na kama urutubishaji haukutokea basi yai lile huharibika na kutoka kwa Njia ya HEDHI au period.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments