Magonjwa
DALILI ZA UKOMO WA HEDHI(Menopause)
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2021/08/images-8.jpeg)
HEDHI
• • • • •
DALILI ZA UKOMO WA HEDHI(Menopause)
Mwanamke ambaye amekaribia ukomo wa hedhi(perimenopause), anaweza kupata dalili mbali mbali na dalili hizo ni kama vile:
-Blid kuanza kutokueleweka kama mwanzoni
– Kuanza kupata tatizo la Ukavu wa uke
– Mwili Kuwaka moto au kuwa na joto sana kuliko kawaida
– Kuhisi Baridi sana mara kwa mara
– Mwili Kutoa sana Jasho wakati wa usiku
– Kuanza kukosa usingizi au kupata Shida ya kulala
– Mood hubadilika
– Kuongezeka kwa uzito wa mwili na kupungua kwa mchakato wa kimetaboliki
– Kuwa na Nywele nyembamba na ngozi kavu
– Kupoteza umbo la matiti,matiti kusinyaa zaidi n.k
– Ishara na dalili, pamoja na mabadiliko katika hedhi vinaweza kutofautiana kati ya mwanamke mmoja na mwingine.
Vipindi vya kuanza kukosa hedhi mara kwa mara kuliko ilivyokawaida vinatarajiwa kutokea. Mara nyingi, vipindi vya hedhi vitaruka mwezi na kurudi, au kuruka miezi kadhaa na kisha kuanza mizunguko ya kila mwezi tena kwa miezi michache.
Vipindi hivi pia huweza kuhusisha kutokea kwa mizunguko mifupi, Licha ya vipindi visivyo vya kawaida, ujauzito pia unawezekana katika kipindi hiki. Hivo ni muhimu pia kuchukua tahadhari kwani uwezo wa mwanamke kutokubeba mimba huanza baada ya kuingia kipindi cha ukomo wa hedhi na sio karibu na ukomo wa hedhi.
Kwa maana nyingine,mwanamke ambaye amekaribia ukomo wa hedhi anaweza kubeba mimba pia.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Magonjwa6 days ago
Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu
-
magonjwa ya wanawake5 days ago
Dalili za Ectopic pregnancy,Mimba kutunga nje ya kizazi
-
Magonjwa2 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri4 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Events1 day ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
Uzazi/Ujauzito11 hours ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Events6 days ago
Princess Anne alilazwa hospitalini na majeraha madogo kufuatia tukio nyumbani kwake
-
News4 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI