magonjwa ya wanawake
DALILI ZA UKOMO WA HEDHI(Menopause)
HEDHI
• • • • •
DALILI ZA UKOMO WA HEDHI(Menopause)
Mwanamke ambaye amekaribia ukomo wa hedhi(perimenopause), anaweza kupata dalili mbali mbali na dalili hizo ni kama vile:
Chat Nasi Whatsapp
"Ungana na Wasomaji zaidi ya 12,000 wanaopata huduma ndani ya afyaclass,Kama unachangamoto yoyote ya kiafya;Kwa Ushauri&Tiba tuwasiliane hapa kupitia WhatSapp,Kama huna Whatsapp tuma SMS au Piga +255758286584."
Chat WhatSapp Hapa-Blid kuanza kutokueleweka kama mwanzoni
– Kuanza kupata tatizo la Ukavu wa uke
– Mwili Kuwaka moto au kuwa na joto sana kuliko kawaida
– Kuhisi Baridi sana mara kwa mara
– Mwili Kutoa sana Jasho wakati wa usiku
– Kuanza kukosa usingizi au kupata Shida ya kulala
– Mood hubadilika
– Kuongezeka kwa uzito wa mwili na kupungua kwa mchakato wa kimetaboliki
– Kuwa na Nywele nyembamba na ngozi kavu
– Kupoteza umbo la matiti,matiti kusinyaa zaidi n.k
– Ishara na dalili, pamoja na mabadiliko katika hedhi vinaweza kutofautiana kati ya mwanamke mmoja na mwingine.
Vipindi vya kuanza kukosa hedhi mara kwa mara kuliko ilivyokawaida vinatarajiwa kutokea. Mara nyingi, vipindi vya hedhi vitaruka mwezi na kurudi, au kuruka miezi kadhaa na kisha kuanza mizunguko ya kila mwezi tena kwa miezi michache.
Vipindi hivi pia huweza kuhusisha kutokea kwa mizunguko mifupi, Licha ya vipindi visivyo vya kawaida, ujauzito pia unawezekana katika kipindi hiki. Hivo ni muhimu pia kuchukua tahadhari kwani uwezo wa mwanamke kutokubeba mimba huanza baada ya kuingia kipindi cha ukomo wa hedhi na sio karibu na ukomo wa hedhi.
Kwa maana nyingine,mwanamke ambaye amekaribia ukomo wa hedhi anaweza kubeba mimba pia.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
Medical Disclaimer
Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.
Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?
💬 Wasiliana na Daktari Hapa

