Ticker

6/recent/ticker-posts

SABABU ZA VIFO VYA WAJAWAZITO



UZAZI/WAJAWAZITO

• • • • • •

SABABU ZA VIFO VYA WAJAWAZITO


Kuna Vifo mbali mbali amabavyo hutokea kwa wakina mama wajawazito,wakati wanajifungua au hata kabla ya muda wa kujifungua kufika,je vifo hivi hutokana na nini? Hizi hapa chini ni baadhi ya sababu za vifo kwa wakina mama wajawazito


- Tatizo la mama kuvuja damu nyingi kupita kiasi wakati na baada ya kujifungua ambapo kwa kitaalam hujulikana kama postpartum hemorrhage(PPH),


Asilimia kubwa ya tatizo hili hutokea ndani ya masaa 24 baada ya mama kujifungua,na vifo vingi ambavyo hutokana na tatizo hili la kuvuja damu nyingi kwa wakina mama hutokea wakati wa kujifungua au muda mfupi tu baada ya kujifungua


- Maambukizi ya magonjwa ambapo hujulikana kama Sepsis au Infection, Pia maambukizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa kama vile Virusi,Bacteria n.k huweza kuchangia vifo kwa wakina mama wajawazito


- Tatizo la Kifafa Cha Mimba, Pia wakina mama wengi hupoteza maisha wakati wa ujauzito kutokana na kupatwa na tatizo la kifafa cha mimba,


Ndyo mana kuna umuhimu mkubwa sana kwa mama mjamzito kuhudhuria kliniki, lakini pia kupata vipimo mbali mbali kama vile; kipimo cha Presha, kupima Uwepo wa Protein kwenye Mkojo n.k ili kama kuna viashiria vyovyote vya tatizo la kifafa cha mimba mama mjamzito aanze kupata msaada mapema.


- Mama kuvuja damu nyingi wakati wa ujauzito kutokana na sababu mbali mbali kama vile;


  • Kupatwa na tatizo la damu kushindwa kuganda yaani Coagulopahty


  • Kondo la nyuma yaani Placenta kuachia sehemu lilipojishikiza ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Placenta abruption


  • Kuvuja damu baada ya kupata ajali, kupigwa,kuanguka n.k


- Mama mjamzito kuwa na matatizo mbali mbali ya Moyo kama vile; Cardiomyopathy,tatizo la mishipa ya damu ndani ya moyo kuziba n.k


- Mama mjamzito kupatwa na tatizo la clots za damu iliyoganda kwenda moja kwa moja kwenye mapafu hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Pulmonary embolism,


Tatizo hili ni hatari sana na huweza kusababisha mama mjamzito kupoteza maisha yake ndani ya muda mfupi


- Mama mjamzito kupatwa na tatizo la maji ya uzazi yaani Amniotic fluid kuingia kwenye mzunguko wa damu hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Amniotic fluid embolism,


Na hiki ndyo chanjo kikubwa cha vifo kwa wakina mama wajawazito ambao wanajaribu Kutoa MIMBA kwa sababu moja au nyingine.


- SABABU ZINGINE NI PAMOJA NA;


  •Tatizo la Presha au shinikizo la damu wakati wa ujauzito


  • Ugonjwa wa kisukari


  • Mimba kutunga nje ya Kizazi yaani Ectopic pregnancy


  • Tumbo la uzazi kupasuka yaani Uterine rupture


  • Mtoto kukaa vibaya tumboni na sababu zingine, japo huchangia kwa asilimia ndogo


  • Kondo la nyuma kushuka chini zaidi ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Placenta praevia, Pamoja na Sababu zingine..!!!



• Soma pia: Sababu za Wanawake Wengi kujifungua kwa upasuaji


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments