Connect with us

magonjwa

Tatizo La Masikio Kupiga Kelele,chanzo na tiba yake(Tinnitus)

Doctor Ombeni

Published

on

246 Views
0 Comments

Tatizo La Masikio Kupiga Kelele,chanzo na tiba yake(Tinnitus)

Tinnitus, Tatizo hili huhusisha mtu kusikia sauti za makelele au kitu kinaita(ringing) ndani ya sikio moja au yote mawili na sauti hizo hazitoki nje na wala hakuna mtu mwingine anazisikia zaidi ya mhusika mwenyewe.

Tatizo hili hutokea kwa watu wengi takribani asilimia 15% mpaka 20%, na hasa kwa watu wenye umri mkubwa au wazee, 

Mtu mwenye tatizo hili huweza kusikia sauti mbali mbali kati ya hizi hapa chini;

– Muito au ringing ndani ya sikio

– Kubweka

– Kunguruma

– Kitu kinagonda ndani ya sikio

– sauti za Kusisimua au kutekenya N.k

CHANZO CHA TATIZO HILI LA TINNITUS

Hakuna sababu moja ambayo inasababisha tatizo hili,ila kuna mjumuisho wa sababu mbali mbali ambazo huongeza uwezekano wa mtu kupatwa na tatizo hili,na sababu hizo ni kama vile;

1. Tatizo la kupoteza usikivu,ambapo seli za vinyeleo ndani ya sikio kwenye sehemu ya ndani(Cochlea) ambazo zinasaidia sikio kupokea mawimbi ya Sauti kwa kupitia Auditory nerves kwenda kwenye ubongo,

Lakini baada ya ubongo kupokea hizo Electrical signals hutafsiri kama kelele badala ya sauti ya kawaida,na ndipo tatizo hutokea.

2. Nywele ndani ya sikio kupinda au kutoka zenyewe kutokana na sababu mbali mbali kama vile umri mkubwa au kuwa katika mazingira ambayo kunakuwa na sauti kubwa sana mara kwa mara kama vile ya muziki n.k, 

hali hii ya kuwa katika mazingira haya ya SAUTI KUBWA SANA inayopenya masikioni huweza kusababisha mtu kuwa na tatizo hili

3. Maambukizi ya vimelea vya magonjwa mbali mbali kwenye sikio kama vile bacteria,Fangasi,Virusi n.k

4. Tatizo la sikio kuziba kutokana na sababu mbali mbali kama vile kuwa na maji mengi sikioni, nta kuzidi(EarWax), uchafu au kitu chochote ambacho kinaweza kuziba sikio lako

5. Kuumia kichwani au shingoni, hali hii huweza kuathiri sikio la ndani, nerves zinazosaidia sikio kusikia pamoja na utendaji kazi wa ubongo

6. Matumizi ya baadhi ya dawa, Mtu kuoverdose dawa au kutumia dawa kwa muda mrefu huweza kusababisha tatizo hili, na hapa tunazungumzia matumizi ya dawa mbali mbali kama vile;

 dawa jamii ya Nonsteroidal anti-inflammatory drugs(NSAIDs), Baadhi ya antibiotics, Dawa za kutibu kansa au saratani, Dawa jamii ya Diuretics, Antidepressants, Dawa za Malaria N.k

7. Matatizo ya muda mrefu yanayohusisha Nerves au mfumo wa Fahamu

8. Magonjwa kama vile Menieres ambayo huweza kusababisha abnormal Inner Ear fluid pressure n.k

9. Kutokufanya kazi vizuri kwa Eustachian tube ndani ya sikio

10. Tatizo kwenye mifupa ya sikio kama vile kukakamaa ndani ya sikio ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Otosclerosis

11. Tatizo la misuli yaani Muscle spasms ndani ya sikio

12. Matatizo kwenye mishipa ya damu ndani ya sikio ambayo huweza kuathiri mzuguko wa damu kwenye sikio, na matatizo hayo ni pamoja na; Atherosclerosis, Shinikizo la Damu(High blood pressure), Kinked, n.k

13. SABABU ZINGINE NI KAMA VILE;

– Ugonjwa wa kisukari

– Matatizo kwenye tezi la Thyroid

– Tatizo la maumivu makali sana ya kichwa cha mara kwa mara au Migraines

– Tatizo la Anemia au upungufu wa damu mwilini

– Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili yaani Autoimmune disorders kama vile; Rheumatoid arthritis, Lupus n.k

MADHARA YA TATIZO HILI NI PAMOJA NA

1. Mwili kuchoka kupita kiasi

2. Kupatwa na tatizo la mfadhaiko,msongo wa mawazo n.k

3. Kupata tatizo la kukosa usingizi

4. Kupata tatizo la kupoteza kumbukumbu

5. Kushindwa kufanya kitu kimoja vizuri na kwa utulivu au kuloose concetration

6. Kuanza kupatwa na tatizo la wasiwasi kila mara

7. Kupata maumivu ya kichwa mara kwa mara n.k

MATIBABU YA TATIZO HILI

Matibabu ya tatizo hilo hutegemea na chanzo chake,hivo kwa ujumla zipo njia mbali mbali za kutibu tatizo hili kama vile;

✓ Kuondoa nta au uchafu wowote ambao umeziba sikio

✓ Kutibu tatizo la mishipa ya damu,tatizo la presha,kisukari n.k

✓ Kuacha baadhi ya dawa au kubadilisha baadhi ya dawa

✓ Kupewa vifaa vya kukusaidia kusikia yaani Hearing aids n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Vitu ambavyo huongeza hatari ya Kupata Tatizo la Kelele Masikioni

1.Kukaa Sehemu Zenye Makelele mengi,

Kelele kubwa, kama vile zile za vifaa vizito,Vyuma kugongwa, misumeno ya minyororo na silaha za moto, ni vyanzo vikubwa vya upotezaji wa kusikia unaohusiana na kelele.

Vifaa vya muziki vinavyotumia Sauti Kubwa Sana, vinaweza pia kusababisha upotevu wa kusikia unaohusiana na kelele kikichezwa kwa sauti kubwa kwa muda mrefu.  Watu wanaofanya kazi katika mazingira yenye kelele – kama vile wafanyikazi wa kiwanda na ujenzi, wanamuziki na wanajeshi – wako hatarini pia kupata tatizo hili la Kelele masikioni.

2. Umri

Unapozeeka, idadi ya nyuzi za neva zinazofanya kazi katika masikio yako hupungua, na hivyo kusababisha matatizo ya kusikia ambayo mara nyingi huhusishwa na tatizo la masikio kupiga kelele au tinnitus.

3. Jinsia

Wanaume wana uwezekano mkubwa wa kupata tatizo la masikio kupiga kelele au tinnitus kuliko wanawake.

4. Matumizi ya Pombe,na Tumbaku.

Wavutaji sigara wana hatari kubwa ya kupata tatizo la masikio kupiga kelele au tinnitus.  Kunywa pombe pia huongeza hatari ya kupata tatizo hili la masikio kupiga kelele tinnitus.

5. Baadhi ya Matatizo ya Kiafya.

 Hapa Nazungumzia matatizo mbali mbali ikiwemo;

  • Tatizo la Uzito mkubwa au Unene(Overweight/Obesity)
  • Matatizo ya Moyo(cardiovascular problems), 
  • Tatizo la Shinikizo la juu la Damu(high blood pressure)
  • Kuwa na historia ya kuumwa tatizo la arthritis
  • Kuumia eneo la kichwani n.k

Jinsi ya Kuzuia Tatizo hili la Masikio kupiga Kelele au Masikio kunguruma

Katika hali nyingi, tatizo la Masikio kunguruma au masikio kupiga kelele(tinnitus) ni matokeo ya kitu ambacho hakiwezi kuzuiwa.  Hata hivyo, baadhi ya tahadhari zinaweza kusaidia kuzuia aina fulani za tinnitus;

Tumia vizuia kelele masikioni

 Baada ya muda, Makelele yatokanayo na sauti kubwa yanaweza kuharibu mishipa katika masikio, na kusababisha hasara ya kusikia na kupata tatizo la masikio kupiga kelele(tinnitus),

Hivo iwapo upo kwenye mazingira yenye kelele kubwa ambazo huwezi kuziepuka Jaribu kupunguza mawimbi makubwa ya sauti kwa kutumia vifaa vya kuzuia kelele masikioni.

 Na ikiwa huwezi kuepuka sauti kubwa, tumia kinga ya Masikio ili kulinda usikivu wako.  Ikiwa unatumia misumeno ya minyororo, ni mwanamuziki, unafanya kazi katika tasnia inayotumia mashine zenye sauti kubwa au kutumia bunduki (hasa bastola au bunduki), kila wakati vaa kinga ya kuzuia Sauti kubwa masikioni.

✓ Epuka mazingira yenye Sauti kubwa

Kama inawezekana kaa mbali na mazingira yenye Sauti kubwa,ikiwemo;

  • Mazingira yenye kelele kubwa za vifaa vya chuma,vyuma kugongwa
  • Misemo inayopiga kelele
  • Mashine za viwandani
  • Muziki mkubwa sana
  • Na aina zingine zote za Kelele kubwa

✓ Punguza sauti

Kukaa kwa muda mrefu kwenye mazingira ya kelele kubwa kama vile muziki mkubwa huweza kuathiri masikio yako na kusababisha tatizo la kelele masikioni,

Hivo kusikia sauti hizi bila ulinzi wa sikio au kusikiliza muziki kwa sauti ya juu sana kupitia vipokea sauti vinavyobanwa kichwani kunaweza kusababisha upotevu wa kusikia na tatizo la tinnitus.

Punguza Sauti kubwa ya Vifaa vya muziki Kama vile Earphone,Sabufa,Spika n.k

 ✓ Linda afya yako kwa Ujumla

Jikinge na matatizo mbali mbali ikiwemo;

  • Tatizo la Uzito mkubwa au Unene(Overweight/Obesity)
  • Matatizo ya Moyo(cardiovascular problems), 
  • Tatizo la Shinikizo la juu la Damu(high blood pressure)
  • Kuwa na historia ya kuumwa tatizo la arthritis
  • Kuumia eneo la kichwani n.k

Fanya Mazoezi ya mara kwa mara, kula Mlo bora kiafya na kuchukua hatua nyingine ili kuweka mishipa yako ya damu kuwa na afya, Hii inaweza kusaidia kuzuia tatizo la tinnitus Linayohusishwa na fetma na matatizo ya mishipa ya damu.

✓ Acha kabsa au Punguza matumizi ya pombe, Sigara,Tumbaku au vitu vyenye kafeini nyingi na nikotini.

Vitu hivi zinapotumiwa kwa kiwango kikubwa, vinaweza kuathiri mtiririko wa damu na kuchangia kwenye tatizo la masikio kupiga kelele au tinnitus.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Links Sources:

  • MayoClinic-https://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/tinnitus/symptoms-causes/syc-20350156
  • ClevelandClinic-https://my.clevelandclinic.org/health/symptoms/14164-tinnitus
  • NIH-https://www.nidcd.nih.gov/health/tinnitus
  • Wikipendia-https://en.wikipedia.org/wiki/Tinnitus

References

  1.  “Tinnitus”National Institute on Deafness and Other Communication Disorders, US National Institutes of Health. 1 May 2023. Retrieved 30 March 2026.
  2.  Baguley D, McFerran D, Hall D (November 2013). “Tinnitus”The Lancet382 (9904): 1600–1607. doi:10.1016/S0140-6736(13)60142-7PMID 23827090.
  3.  Han BI, Lee HW, Kim TY, Lim JS, Shin KS (March 2009). “Tinnitus: characteristics, causes, mechanisms, and treatments”Journal of Clinical Neurology5 (1): 11–19. doi:10.3988/jcn.2009.5.1.11PMC 2686891PMID 19513328About 75% of new cases are related to emotional stress as the trigger factor rather than to precipitants involving cochlear lesions.
  4.  Langguth B, Kreuzer, PM, Kleinjung, T, De Ridder, D (September 2013). “Tinnitus: causes and clinical management”. The Lancet Neurology12 (9): 920–930. doi:10.1016/S1474-4422(13)70160-1PMID 23948178S2CID 13402806.
  5.  Levine RA, Oron Y (2015). “Tinnitus”. The Human Auditory System – Fundamental Organization and Clinical Disorders. Handbook of Clinical Neurology. Vol. 129. pp. 409–431. doi:10.1016/B978-0-444-62630-1.00023-8ISBN 978-0-444-62630-1PMID 25726282.
  6.  Jarach CM, Lugo A, Scala M, van den Brandt PA, Cederroth CR, Odone A, Garavello W, Schlee W, Langguth B, Gallus S (1 September 2022). “Global Prevalence and Incidence of Tinnitus: A Systematic Review and Meta-analysis”JAMA Neurology79 (9): 888–900. doi:10.1001/jamaneurol.2022.2189ISSN 2168-6149PMC 9361184PMID 35939312.
  7.  Salazar JW (2019). “Depression in Patients with Tinnitus: A Systematic Review”Otolaryngol Head Neck Surg161 (1): 28–35. doi:10.1177/0194599819835178PMC 7721477PMID 30909841.
  8.  Bhatt JM (2016). “Relationships Between Tinnitus And The Prevalence Of Anxiety And Depression”Laryngoscope127 (2): 466–469. doi:10.1002/lary.26107PMC 5812676PMID 27301552.
  9.  Esmaili AA, Renton J (1 April 2018). “A review of tinnitus”Australian Journal of General Practice47 (4): 205–208. doi:10.31128/AJGP-12-17-4420PMID 29621860.
  10.  Mazurek B, Haupt H, Olze H, Szczepeck A (2022). “Stress and tinnitus—from bedside to bench and back”Frontiers in Systems Neuroscience6 (47): 47. doi:10.3389/fnsys.2012.00047PMC 3371598PMID 22701404.
  11.  Henry JA, Dennis KC, Schechter MA (October 2005). “General Review of Tinnitus: Prevalence, Mechanisms, Effects, and Management”. Journal of Speech, Language, and Hearing Research48 (5): 1204–1235. doi:10.1044/1092-4388(2005/084)PMID 16411806.
  12.  Rizk HG, Lee JA, Liu YF, Endriukaitis L, Isaac JL, Bullington WM (December 2020). “Drug-Induced Ototoxicity: A Comprehensive Review and Reference Guide”. Pharmacotherapy40 (12): 1265–1275. doi:10.1002/phar.2478PMID 33080070S2CID 224828345.
  13.  Simmons R, Dambra C, Lobarinas E, Stocking C, Salvi R (2008). “Head, Neck, and Eye Movements That Modulate Tinnitus”Seminars in Hearing29 (4): 361–370. doi:10.1055/s-0028-1095895PMC 2633109PMID 19183705.
  14.  Baguley D, Andersson g, McFerran D, McKenna L (2013). Tinnitus: A Multidisciplinary Approach (2nd ed.). Blackwell Publishing Ltd. pp. 16–17. ISBN 978-1-118-48870-6.
246 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

LATEST POSTS

magonjwa1 year ago

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba Genital warts ni ugonjwa gani,Soma Zaidi hapa kufahamu Genital warts ni moja ya aina...

magonjwa2 years ago

Vipele Sehemu Ya Siri,Vipele Ukeni, Vipele Kwenye Uume

VIPELE SEHEMU YA SIRI,VIPELE UKENI, VIPELE KWENYE UUME Vipele kwenye Uume: Vipele Kwenye Uume: Chanzo, Dalili na Matibabu Tatizo la...

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips1 day ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti1 day ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

247
0