Connect with us

Magonjwa

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

Avatar photo

Published

on

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

tatizo la masikio kupiga kelele

Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele, mtu husikia sauti za makelele au kitu kinaita(ringing) ndani ya sikio moja au yote mawili na sauti hizo hazitoki nje na wala hakuna mtu mwingine anazisikia zaidi ya mhusika mwenyewe.

Je unasumbuliwa sana na tatizo la Masikio kupiga kelele? haupo peke yako

Tatizo la masikio kupiga kelele hutokea kwa watu wengi takribani asilimia 15% mpaka 20%, na hasa kwa watu wenye umri mkubwa au wazee, Mtu mwenye tatizo hili la masikio kupiga kelele huweza kusikia sauti mbali mbali kati ya hizi hapa chini;

  • Muito au ringing ndani ya sikio
  •  Kubweka
  • Kunguruma
  •  Kitu kinagonga ndani ya sikio
  • sauti za Kusisimua au kutekenya N.k

CHANZO CHA TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE(TINNITUS)

Hakuna sababu moja ambayo inasababisha tatizo La masikio kupiga kelele,ila kuna mjumuisho wa sababu mbali mbali ambazo huongeza uwezekano wa mtu kupatwa na tatizo hili,na sababu hizo ni kama vile;

1. Tatizo la kupoteza usikivu,ambapo seli za vinyeleo ndani ya sikio kwenye sehemu ya ndani(Cochlea) ambazo zinasaidia sikio kupokea mawimbi ya Sauti kwa kupitia Auditory nerves kwenda kwenye ubongo,

Lakini baada ya ubongo kupokea hizo Electrical signals hutafsiri kama kelele badala ya sauti ya kawaida,na ndipo tatizo la masikio kupiga kelele hutokea.

2. Nywele ndani ya sikio kupinda au kutoka zenyewe kutokana na sababu mbali mbali kama vile umri mkubwa au kuwa katika mazingira ambayo kunakuwa na sauti kubwa sana mara kwa mara kama vile ya muziki n.k,

hali hii ya kuwa katika mazingira haya ya SAUTI KUBWA SANA inayopenya masikioni huweza kusababisha mtu kuwa na tatizo la masikio kupiga kelele

3. Maambukizi ya vimelea vya magonjwa mbali mbali kwenye sikio kama vile bacteria,Fangasi,Virusi n.k

4. Tatizo la sikio kuziba kutokana na sababu mbali mbali kama vile kuwa na maji mengi sikioni, nta kuzidi(EarWax), uchafu au kitu chochote ambacho kinaweza kuziba sikio lako

5. Kuumia kichwani au shingoni, hali hii huweza kuathiri sikio la ndani, nerves zinazosaidia sikio kusikia pamoja na utendaji kazi wa ubongo

6. Matumizi ya baadhi ya dawa, Mtu kuoverdose dawa au kutumia dawa kwa muda mrefu huweza kusababisha tatizo la masikio kupiga kelele,

na hapa tunazungumzia matumizi ya dawa mbali mbali kama vile;

  • dawa jamii ya Nonsteroidal anti-inflammatory drugs(NSAIDs),
  • Baadhi ya antibiotics,
  • Dawa za kutibu kansa au saratani,
  • Dawa jamii ya Diuretics, Antidepressants,
  • Kuoverdose Dawa za Malaria kama quinine N.k

7. Matatizo ya muda mrefu yanayohusisha Nerves au mfumo wa Fahamu, pia huweza kuwa chanzo cha tatizo la Masikio kupiga kelele

8. Magonjwa kama vile Menieres ambayo huweza kusababisha abnormal Inner Ear fluid pressure n.k

9. Kutokufanya kazi vizuri kwa Eustachian tube ndani ya sikio

10. Tatizo kwenye mifupa ya sikio kama vile kukakamaa ndani ya sikio ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Otosclerosis

11. Tatizo la misuli yaani Muscle spasms ndani ya sikio, Pia huweza kuongeza hatari ya mtu kupata tatizo la masikio kupiga kelele

12. Matatizo kwenye mishipa ya damu ndani ya sikio ambayo huweza kuathiri mzuguko wa damu kwenye sikio, na matatizo hayo ni pamoja na; Atherosclerosis, Shinikizo la Damu(High blood pressure), Kinked, n.k

13. SABABU ZINGINE Za Tatizo la Masikio kupiga Kelele NI KAMA VILE;

– Ugonjwa wa kisukari

– Matatizo kwenye tezi la Thyroid

– Tatizo la maumivu makali sana ya kichwa cha mara kwa mara au Migraines

– Tatizo la Anemia au upungufu wa damu mwilini

– Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili yaani Autoimmune disorders kama vile; Rheumatoid arthritis, Lupus n.k

Vyote hivi huweza kuongeza hatari ya mtu kupata tatizo la Masikio kupiga kelele

MADHARA YA TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE NI PAMOJA NA;

1. Mwili kuchoka kupita kiasi

2. Kupatwa na tatizo la mfadhaiko,msongo wa mawazo n.k

3. Kupata tatizo la kukosa usingizi

4. Kupata tatizo la kupoteza kumbukumbu

5. Kushindwa kufanya kitu kimoja vizuri na kwa utulivu au kuloose concetration

6. Kuanza kupatwa na tatizo la wasiwasi kila mara

7. Kupata maumivu ya kichwa mara kwa mara n.k

MATIBABU YA TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE

Matibabu ya tatizo la masikio kupiga kelele hutegemea na chanzo chake,hivo kwa ujumla zipo njia mbali mbali za kutibu tatizo hili la masikio kupiga kelele kama vile;

âś“ Kuondoa nta au uchafu wowote ambao umeziba sikio

âś“ Kutibu tatizo la mishipa ya damu,tatizo la presha,kisukari n.k

âś“ Kuacha baadhi ya dawa au kubadilisha baadhi ya dawa

âś“ Kupewa vifaa vya kukusaidia kusikia yaani Hearing aids n.k

Hitimisho

Tatizo la Masikio kupiga kelele huweza kusababishwa na sababu mbali mbali ikiwemo; Kuoverdose baadhi ya dawa kama vile dawa za Malaria mfano Quinine n.k

Kama unatatizo hili hakikisha unafanya vipimo na kupata Tiba au,

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa5 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa6 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...