Ticker

6/recent/ticker-posts

 


Dalili za mwanzo za kisukari kwa mwanaume



Dalili za mwanzo za kisukari kwa mwanaume

Kuna ishara nyingi za tahadhari zinazotokea mapema pamoja na dalili za mwanzo kabsa za ugonjwa wa kisukari kwa wanaume.

Kwa vyovyote vile, wasiliana na daktari na usiwahi kutumia dawa wewe mwenyewe, kwa sababu inaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi.

Hizi hapa ni baadhi ya Dalili za mwanzo za kisukari kwa mwanaume;

1. Kuwa na Kiu pamoja na njaa kupita kiasi(Excessive Thirst and Hunger)

Kwa kuwa kiwango cha sukari kwenye damu ni kikubwa, huvuta maji kutoka kwenye seli na kumfanya mgonjwa ahisi kiu kupita kiasi.

Watu wanaougua kisukari huhisi njaa mara kwa mara kwa sababu ya Mwili kutoweza kutumia ipasavyo sukari ya damu kwa kuigeuza kuwa nishati. Ikiwa unajikuta unakunywa galoni za maji au unaanza kula chakula ghafla mara kwa mara na kuhisi njaa kila wakati, zungumza na daktari wako.

2. Kukojoa mara kwa mara(Frequent Urination)

Watu wanaougua ugonjwa wa sukari huanza kukojoa mara kwa mara. Kiu nyingi,kunywa maji mengi,husababisha kukojoa mara kwa mara, na Wanaume wengi wanakabiliwa na shida ya kupata usingizi mzuri usiku.

Wagonjwa wazee wanaweza hata kupata shida ya kukojoa kitandani. Mwili hujaribu kutoa glucose ya ziada katika damu kupitia mkojo. Hiyo ni sababu nyingine ya kukojoa mara kwa mara.

3. Mwili kuchoka kupita kiasi

Iwapo kwa ujumla umekuwa ukijihisi kuchoka sana na kuteseka kutokana na uchovu bila sababu zozote zinazoeleweka, unaweza kuwa na kisukari.(Ingawa KiSukari sio sababu pekee ya wewe kuchoka sana, hata magonjwa mengine na sababu zingine huweza kupelekea shida hii)

Uchovu usioelezeka kwa mgonjwa wa Sukari ni kwa sababu ya matumizi duni ya nishati. Kipimo cha Sukari(glukosi) kitakupa majibu kwa hivyo fanya vipimo mara moja.

4.Uzito kupungua kwa kasi sana pasipo na sababu inayoeleweka

Men suffering from diabetes undergo unexplained weight loss. The body is unable to use blood sugar to transform it into energy. This leads to sudden weight loss. If you have lost weight without any reason, please consult your doctor.

5. Kupata maambukizi ya ngozi mara kwa mara(Skin Infections)

Kwa sababu ya kiwango cha sukari kwenye damu kuwa Juu, wanaume wanaougua ugonjwa wa kisukari hupata maambukizi ya ngozi mara nyingi sana.

Hali Hii inaweza kusababisha kuwashwa kwenye sehemu za siri au hata kupata fangasi kwa urahisi(thrush),

Sukari ikiwa juu hutengeneza mazingira mazuri ya kuzaliana kwa fangasi ambao husababisha maambukizo haya.

6. Kupata matatizo ya macho kutokuona vizuri

Wanaume wanaougua kisukari hupata uoni hafifu na kupoteza uwezo wa kuona kwa ujumla,

Viwango vya juu vya sukari mwilini ni hatari kwa viungo vingi lakini macho huwa ya kwanza kuumia. Tafuta matibabu mara moja ikiwa umepata shida ya macho kutokuona vizuri kwa gafla.

7. Vidonda kuchelewa Kupona

Wanaume wanaougua ugonjwa wa kisukari hupata majeraha/vidonda kwa urahisi na majeraha yao huchukua muda kupona.

Sukari nyingi katika damu hupunguza kinga na huathiri uwezo wa mwili wa kujiponya,

Kwa kuwa hali hiyo inaweza kuzidisha tatizo la gangrene na hata kupelekea mtu kukatwa viungo, ikiwa una jeraha ambalo haliponi, tafuta ushauri wa kitabibu.

8. Kupata Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume(Erectile Dysfunction)

Kisukari hasa aina ya 2 kwa kawaida huhusishwa na tatizo la uume kushindwa kusimama vizuri au uume kutokusimama kabsa(erectile dysfunction), kwani uwepo wa sukari nyingi kwenye damu kwa muda mrefu huweza kuharibu mishipa ya fahamu na mishipa ya damu na kusababisha matatizo ya uume kushindwa kusimama kabsa au kushindwa kusimama vya kutosha.

Wanaume wanaougua ugonjwa wa kisukari hupata shida ya nguvu za kiume kutokana na mzunguko mdogo wa damu kwenye viungo kama vile eneo la pelvisi.

Vitu hivi huongeza hatari ya Kupata Ugonjwa wa Kisukari kwa Mwanaume

Sababu nyingi huchangia au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa wa kisukari na matatizo yanayohusiana na ugonjwa huu, baadhi ya Sababu hizo ni pamoja na:

  • Kuongezeka Uzito kwa haraka sana(Uzito mkubwa kupita kiasi)
  • Uvutaji wa Sigara
  • Unywaji wa Pombe kupita kiasi
  • Kuwa na shida ya presha kubwa kwenye damu(High blood pressure)
  • Kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu mwilini(high cholesterol)
  • Kutokufanya mazoezi ya mwili
  • Kuwa na umri wa Zaidi ya miaka 45 n.k

Jikinge na Ugonjwa wa Kisukari kwa kufanya haya

✓ Epuka kabsa Uvutaji wa Sigara

✓ Epuka matumizi ya pombe kupita kiasi

✓ Hakikisha unadhibiti Uzito wako wa mwili na kuepuka kuwa na Uzito kupita kiasi

✓ Fanya Mazoezi mbali mbali ya Mwili angalau kwa dakika 30(nusu saa) kila siku

✓ Kula Mlo bora kwa afya yako, Epuka ulaji wa vitu vya sukari nyingi,chumvi nyingi au mafuta mengi sana.n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments