Ticker

6/recent/ticker-posts

Muda sahihi wa kusoma kipimo cha ukimwi



Nmekuwa nikipata simu nyingi na maswali mengi juu ya shida hii…

Watu wengi wanajipima HIV wanaona kipimo chao kimesoma line moja ya C-Control ikiwa na maana ya NEGATIVE, lakini baada ya Muda wanaona kuna Mstari Zaidi ya Mmoja, hali ambayo inafawanya kupaniki sana na kuwa na hofu kubwa, wakihisi tayari wana maambukizi.

Je ni nini cha kufanya au unakosema wapi? au je tayari una maambukizi?

Zingatia vitu hivi Muhimu sana wakati unajipima mwenyewe HIV;

✓ hakikisha umeangalia Expire date ya kipimo chako,

Unaweza usipate majibu sahihi ikiwa kipimo chako kimeshakwisha muda wake wa matumizi.

✓ Sababu nyingine ya Msingi sana ni Muda wa Kusoma majibu yako,

Muda sahihi wa kusoma kipimo chako cha ukimwi ni kuanzia dakika 10, 15 mpaka 20.

Na baadhi ya Vipimo utakuta wamekuandikia kabsa na Muda wa Kusoma majibu yako, Hakikisha unazingatia sana hili.

Ukisoma Majibu yako Nje ya Muda unaotakiwa, Hapa ndipo Makosa(Error) hutokea kwenye Kipimo chako, na Kuanza kupata majibu ambayo sio sahihi,

Unaweza kupata Majibu kana kwamba Tayari umeshaathirika kumbe Sio, Swala ni muda wa kusoma majibu.

Mwingine anaweza kujipima Sasa hivi Mstari mmoja ukatokea, anakuja Kusoma Majibu yake kesho anakuta kuna Mistari miwili kana kwamba tayari kaathirika.

Zingatia Muda….!!!!

Soma Zaidi Hapa Jinsi ya Kusoma Kipimo cha HIV;



Post a Comment

0 Comments