Ticker

6/recent/ticker-posts

Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani



Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani.

Miami, Florida:

Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti tukio la kusikitisha la kifo cha Mtanzania aliyekuwa akifanya kazi Google.

Mwili wa Mtanzania aliyeanguka kutoka kwenye boti iliyokodishwa aliyokuwa amepanda katika Mto Miami nchini Marekani mwishoni mwa juma umepatikana ukielea majini.

Abraham Mgowano, 35, ambaye alifanya kazi kama mhandisi wa programu za Google, alipatikana Jumanne baada ya kupotea tangu aanguke kutoka kwenye boti ya urefu wa futi 44 ya Sea Ray cabin cruiser siku ya Jumamosi.



Post a Comment

0 Comments