Ticker

6/recent/ticker-posts

Wengine 9 kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Uvimbe kwenye Ubongo



Wengine 9 kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Uvimbe kwenye Ubongo.

WAGONJWA 9 KUFANYIWA UPASUAJI MPYA WA KUONDOA UVIMBE KWENYE UBONGO.

Na Abdallah Nassoro-MOI

Madaktari bingwa wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na madaktari bingwa wabobezi kutoka Chuo Kikuu cha Colorado cha nchini Marekani wanatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa Tisa wenye matatizo ya uvimbe kwenye Ubongo kwa njia ya kisasa ya kutoboa tundu ndogo bila ya kufungua fuvu katika kambi ya mafunzo ya wiki moja inayoendelea MOI jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo wa tatu wa kimataifa wa mafunzo ya matibabu ya kisasa upasuaji wa uvimbe kwenye ubongo yanalenga kubadilishana uzoefu na kuwajengea uwezo madaktari bingwa wazawa, wauguzi wabobezi na wataalam wengine umefunguliwa leo Februari, 19, 2024 na na muwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Lemeri Mchome.

“Mwaka 2017 tulianza upasuaji wa uvimbe vya chini ya ubongo(Pituitary tumors) bila kupasua fuvu kwa mara ya kwanza. Madaktari wa MOI baada ya mafunzo na mashirikiano hayo wameendelea na upasuaji huo mpaka sasa kwa ufanisi mkubwa…

Kwa sasa hapa MOI takribani wagonjwa 572 tunawafanyia upasuaji wa vivimbe kwenye ubongo na karibia asilimia nne ya wagonjwa hawa bado wanaenda nje ya nchi kupata matibabu kwa vivimbe vilivyo ndani kabisa ya ubongo ambapo upasuaji wa kawaida unaweza kuleta madhara zaidi.

Hivyo mafunzo haya yatasadia uanzishwaji wa huduma hii mpya ya upasuaji wa uvimbe ndani ya ubongo (Stereotactic procedures).



Post a Comment

0 Comments