Ticker

6/recent/ticker-posts

Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito



Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito.

Swala la kuvimba miguu kwa mama mjamzito ni kawaida, na hii hutokana na kiwango Zaidi cha maji kujikusanya sehemu za chini ya mwili kama vile kwenye miguu,

Hali hii hutokea hasa ukiwa kwenye hali ya Joto, Umesimama kwa muda mrefu au kukaa kwa muda mrefu.

Pia mgandamizo au pressure ya kiumbe kinachokuwa tumboni huweza kuathiri mtiririko wa damu kwenye miguu yako. Hali hii inaweza kupelekea maji Zaidi kujikusanya kwenye miguu na kusababisha tatizo la miguu kuvimba.

Kuvimba kwa miguu (edema) ni jambo la kawaida kwa wanawake wajawazito, hasa katika trimester ya mwisho.

ANGALIZO; kuvimba miguu sana sio hali ya kawaida,hii inaweza kuwa kiashiria mojawapo cha matatizo ya Ujauzito kama vile; Kifafa cha Mimba

Hata hivyo, kuna njia kadhaa ambazo mama mjamzito anaweza kutumia kudhibiti hali hii ya kuvimba Miguu:

Jinsi ya kudhibiti hali ya kuvimba miguu kwa mama mjamzito.

– Punguza muda wa kusimama:

Jaribu kupunguza muda unaotumia kusimama mfululizo. Kama kazi yako inahitaji usimame sana,

jaribu kutafuta muda wa kukaa chini au kutembea kidogo kusaidia kusukuma damu iliyoko kwenye miguu kurudi juu.

– Pumzika na miguu iwe juu:

Unapopata nafasi ya kupumzika, lala chali na weka miguu yako juu kwa kutumia mto. Hii inasaidia kurudisha damu kwenye mzunguko na kupunguza uvimbe.

– Fanya Mazoezi ya Mwili:

Mazoezi mepesi, kama vile kutembea, kuogelea, au yoga wakati wa Ujauzito, yanaweza kusaidia kuboresha mzunguko wa damu na kupunguza uvimbe.

– Vaa viatu visivyokubana Sana:

Viatu vinavyokubana sana vinaweza kuzuia mzunguko wa damu na kusababisha miguu kuvimba zaidi.

Vaa viatu ambavyo havikubani ili kutoa nafasi ya miguu kupanuka.

Epuka kabsa kuvaa viatu virefu maarufu kama “high heels”.

– Epuka kuvaa nguo zinazobana sana:

Nguo zinazobana sana, hasa kwenye kiuno na miguu, zinaweza kuzuia mzunguko wa damu na kuchangia katika uvimbe wa Miguu.

– Kula chakula chenye afya:

Kula chakula chenye afya, kikiwa na virutubisho kama vile potassium nyingi,mfano kama vile ndizi, na kupunguza ulaji wa chumvi kunaweza kusaidia kudhibiti uvimbe wa miguu.

– Kunywa maji mengi:

Kunywa maji ya kutosha kunaweza kusaidia kutoa sodiamu na toxini nyingine mwilini ambazo zinaweza kuchangia uvimbe wa miguu.

– Usikunje miguu unapokaa:

Kukunja miguu ukiwa umekaa,maarufu kama kukunja NNE,kunaweza kuzuia mzunguko wa damu na kusababisha miguu kuvimba.

– Massage:

Massage ya miguu na miguu inaweza kusaidia kuboresha mzunguko wa damu na kupunguza uvimbe wa miguu.

NB: Ikiwa uvimbe unazidi zaidi kwa ghafla, au unahusishwa na dalili nyingine kama maumivu makali, kuchanganyikiwa, au matatizo ya kuona, ni muhimu sana kuwasiliana na daktari wako mara moja kwani hii inaweza kuwa ishara ya preeclampsia, hali ya hatari inayohitaji uangalizi wa daktari.

AU KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KUPITIA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments