Ticker

6/recent/ticker-posts

Gharama za upasuaji wa kurekebisha maumbile zinaanzia Sh15 milioni hadi Sh22.5 milioni



Gharama za upasuaji wa kurekebisha maumbile zinaanzia Sh15 milioni hadi Sh22.5 milioni.

Wakati Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila ikitarajia kufanya upasuaji wa kurekebisha maumbile Mei 2024, imeelezwa wanawake wenye uhitaji wa huduma hiyo ni wengi, lakini wanakwamishwa na kipato.

Daktari bingwa wa upasuaji wa kurekebisha maumbile kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Erick Muhumba akizungumza na Mwananchi Digital hivi karibuni amesema gharama za upasuaji zinaanzia Sh15 milioni hadi Sh22.5 milioni sawa na Dola za 6,000 za Marekani hadi Dola 9,000 za Marekani.

Upasuaji huo ni pamoja na kuongeza makalio, matiti na kupunguza tumbo.

Dk Muhumba amesema kambi maalumu ya siku tatu kwa ajili ya upasuaji huo inatarajiwa kufanyika Mei 13 hadi 15, 2024.

“Wanaojitokeza na kulipia huduma ni wachache, mpaka sasa kwa kambi ijayo aliyelipia ni mmoja lakini kwa walioonyesha nia ya kulipa ili wapatiwe huduma wapo sita,” amesema Dk Muhumba.

“Wanaoulizia huduma ni wengi, wengine wanakuja wanauliza gharama baada ya kuelezwa wanasema hawana fedha. Tunazungumza nao na tumeshawapatia control number (namba ya malipo) ili wafanye malipo watakapokuwa tayari.”

Dk Muhumba amesema wamesogeza huduma kwa kuwa awali, Watanzania wengi walienda nje ya nchi.

Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi

(Imeandikwa na Herieth Makwetta)

#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa



Post a Comment

0 Comments