Ticker

6/recent/ticker-posts

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho



Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa ni vigumu kutibika.

Glaucoma ni ugonjwa ambao unazidi kuenea katika siku za hivi karibuni. Na ni vigumu kupata kuona tena baada ya kupata ugonjwa huu.

Glaucoma ni ugonjwa unaoathiri macho. Ugonjwa huu huathiri mishipa inayounganisha macho na ubongo. Husababishwa na umajimaji unaojikusanya kwenye jicho na kuziharibu mishipa hiyo.

Wagonjwa wa glaucoma huanza kuwa na matatizo ya kuona na isipogunduliwa na kutibiwa mapema, uwezo wa kuona unaweza kupotea kabisa.

Ugonjwa huu huathiri watu wa rika zote, lakini hatari zaidi ipo kwa watu wenye umri wa miaka 70 hadi 80.

Pia unaweza kusoma

Ishara 4 zinazoonyesha kuwa unahitaji miwani mpya kwa matatizo ya macho20 Mei 2023

Mlemavu wa macho aliyenyimwa elimu awa bilionea13 Februari 2022

Dalili za glaucoma ni nini?

Moja ya matatizo yanayohusiana na ugonjwa huu ni kwamba hakuna dalili za wazi katika hatua za mwanzo na njiia pekee nikufaya vipimo hospitali.

Kuna wakati mtu aliyeathiriwa hawezi kuona chochote. Kutoona vizuri au kuona miduara inayofanana na upinde wa mvua karibu na mwanga ni miongoni mwa dalili za glaucoma.

Ingawa ugonjwa unaweza kuathiri macho yote mawili, lakini mara nyingi ni jicho moja tu linaweza kuathiriwa. Baadhi ya dalili ni:

Maumivu makali machoni

Kuhisi kichefuchefu na kutapika

Macho kuwa mekundu

Maumivu ya kichwa

Maumivu pembeni ya macho

Kutoona vizuri

Kwa hiyo, ikiwa unahisi mojawapo ya dalili zilizo hapo juu, usizipuuze na nenda hospitali mara moja kaonane na daktari.

Ni muhimu sana kutambua na kutibu glakoma katika hatua zake za mwanzo, vinginevyo kuna hatari ugonjwa huo kukuwa na kusababisha kutoona.

Waliohatarini kupata ugonjwa

Umri, licha ya ukweli kuwa wapo watu wa miaka 40 hupata. Lakini ugonjwa huu mara nyingi huwaathiri watu wa miaka 70 na 80.

Watu wenye asili ya Kiafrika na Asia wana uwezekano mkubwa wa kupata glukoma.

Kurithi pia ni sababu, ikiwa mmoja wa wazazi au ndugu zako wamekuwa na ugonjwa huo, basi kuna uwezekano mkubwa nawe kupata ugonjwa huo.

Matatizo ya moyo ni hatari nyingine. Watu walio na kisukari au matatizo mengine ya kuona pia wana uwezekano mkubwa wa kupata glakoma.

Matibabu na Kujikinga

Bado haijajulikana kwa uhakika ni ipi njia bora ya kuzuia glaucoma, lakini uchunguzi wa mara kwa mara wa macho unaweza kuzuia ugonjwa huu na unaweza kutibiwa mapema.

Faida ya uchunguzi wa macho mara kwa mara ni kwamba ugonjwa unaweza kugunduliwa hata bila dalili na hivyo inashauriwa kufanya uchunguzi wa macho kila baada ya miaka miwili.

Ikiwa mtu hupoteza maono kutokana na glaukoma, maono yake hayawezi kurejeshwa, lakini ikiwa maono yanaathiriwa kwa kiasi kidogo, matibabu yanaweza kuzuia uharibifu zaidi.

Matibabu ya glakoma hutegemea aina na kwa kawaida huhusisha kutumia matone maalum ili kupunguza athari kwenye jicho.

Kwa kuongezea, mionzi inaweza kutumika kuondoa kizuizi katika mishipa ya kwenye jicho, pamoja na upasuaji.

#SOMA ZAIDI Ugonjwa huu wa glaucoma hapa



Post a Comment

0 Comments