Connect with us

Magonjwa

je ugonjwa wa pumu unaambukiza

Avatar photo

Published

on

je ugonjwa wa pumu unaambukiza?

Hili ni Swali ambalo watu wengi huuliza,hata kwenye page za afyaclass, kwa kuliona hilo, tumeona kuna haja ya kukusaidia kujua kuhusu ugonjwa huu wa Pumu.

Pumu au kwa jina lingine Asthma ni ugonjwa/hali inyoathiri na kupunguza uwezo wa mapafu kufanya kazi, kwa kusababisha Njia ya hewa kuwa nyembamba na kuvimba.

Kwa kawaida, mara nyingi huonekana kwanza katika utoto na kuathiri watoto na watu wazima, na karibu watu milioni 25.

Fahamu,Sababu za kimazingira kama vile kukabiliwa na vumbi au moshi zinaweza kusababisha mashambulizi ya pumu kwa baadhi ya watu.

Vichochezi tofauti vinaweza kuleta aina tofauti za pumu. Aina hizo pamoja na:

  • adult-onset asthma
  • exercise-induced bronchoconstriction (EIB)
  • occupational asthma
  • asthma-COPD overlap
  • nonallergic asthma
  • allergic asthma
  • Na pediatric asthma

je ugonjwa wa pumu unaambukiza

Je, pumu inaambukiza kwa binadamu?

Pumu haiambukizwi kwa binadamu. Hata hivyo, wataalam wamegundua kwamba pumu huelekea kutokea katika familia,

Kwa hiyo, watoto wa wazazi walio na pumu wako kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa pumu.

Baadhi ya dalili za pumu zinaweza kufanana na hali zinazoweza kuambukizwa (kuambukiza), kama vile tatizo la bronchitis au nimonia. Hata hivyo, ingawa watu walio na dalili za pumu kama kikohozi kinachoendelea wanaweza kuonekana kuwa wagonjwa, pumu haisambai kutoka kwa mtu hadi mtu.

Sababu nyingi zinaweza kusababisha mtu kupata pumu au kusababisha shambulio la pumu. Wakati wa shambulio la pumu, mtu anaweza kupata dalili kali kama vile kupumua kwa shida, kikohozi cha kudumu, au kubana kwa kifua.

Fahamu; Sababu tofauti za kimazingira kama vile kukaa kwenye Mazingira ya vumbi au moshi zinaweza kusababisha mashambulizi ya ghafla ya pumu kwa baadhi ya watu.

Chanzo cha Ugonjwa wa Pumu na Sababu hatarishi za kupata Pumu

Vitu hivi huongeza hatari ya wewe kupata Ugonjwa wa Pumu;

1. Sababu za Kigenetiki

Jenetiki na epigenetics,
Katika miongo michache iliyopita, wanasayansi wameanzisha alama za jeni kadhaa ambazo zinahusishwa na pumu ya utotoni na pumu ya atopiki.

Ingawa, wataalamu pia wanakubali kwamba chembe za urithi ni sababu moja tu ya kuamua hatari ya mtu kupata pumu. Bado inahitajika utafiti Zaidi kuhusu epijenetiki, au jinsi jeni fulani unazobeba zinaweza kuwashwa na kuzimwa kulingana na mazingira yako,

Tafifi zimepata jeni kadhaa ambazo zinahusishwa na kutokea kwa ugonjwa wa pumu – Na pia zipo baadhi ya jeni zinaweza kuwa kinga dhidi ya pumu.

2. Tatizo la Mzio au Allergies

Mzio ni mojawapo ya vichochezi vikubwa vya dalili za pumu. Mwili wako huweza kuleta reactions kwa vitu mbali mbali kama vile ukungu,wadudu, vumbi, nyama,mafuta,n.k kwa kuamsha mfumo wa kinga ya mwili wako kufanya kazi.

Wakati mfumo wako wa kinga unapochochewa na vitu hivo(allergener), inaweza kusababisha uvimbe katika njia ya hewa ya mapafu yako, na kuifanya iwe vigumu kupumua.

3. Uchafuzi wa hewa, Kuwa kwenye mazingira ya Moshi n.k

Ubora wa hewa na mazingira kwa ujumla,
Pumu huathiri vibaya baadhi ya Watu  ambao – kutokana na ubaguzi wa kimfumo – wana uwezekano mkubwa wa kuishi na kufanya kazi karibu na uchafuzi hatari wa hewa.

Aina hii ya uchafuzi wa mazingira inajulikana kuongeza kwa kasi hatari ya mtu kupata pumu.

4.Mabadiliko ya hali ya hewa

Wanasayansi wanaochunguza uhusiano kati ya afya ya binadamu na mazingira wamegundua kuwa athari za mabadiliko ya hali ya hewa, kama vile theluji kuongezeka, mvua, na mafuriko, zinahusishwa na hatari ya kupata Ugonjwa wa pumu..

5. Vichocheo vya Mwili au Hormones

Inaonekana kwamba homoni za jinsia ya kike zinaweza pia kuchangia katika hatari ya mtu kupata pumu. Tafiti zinaonyesha Viwango vya pumu vimeenea zaidi kwa wanawake walioko kwenye umri wa kubalehe na kuendelea.

Viwango vya pumu ni vya juu zaidi kwa wanawake waliopata hedhi za mapema na mimba nyingi, na Hii inafanya Tafiti kupendekeza kipengele cha homoni za jinsia ya kike katika kupata pumu.

Wakati homoni za kike zinapoongezeka, kama vile wakati wa hedhi na ujauzito, hatari ya kupata pumu inaweza kuongezeka. Homoni hizi zinaweza kuongeza uvimbe katika mwili, na kuathiri njia ya hewa.

6. Unene au Uzito Mkubwa(Obesity/Overweight)

Wanasayansi wamegundua kuwa Unene au Obesity ni sababu nyingine inayoweza kuongeza hatari ya mtu kupata pumu. Haijulikani jinsi hali hizi mbili zimeunganishwa, ingawa wataalam wanafikiri inahusiana na kuvimba na kupunguza uwezo wa mapafu kufanya kazi,hali inayosababishwa na uzito Kuzidi.

7. Kupata Maambukizi kwenye Mapafu(Lung infections)

Maambukizi kwenye Mapafu kama vile; RSV,Chlamydia pneumoniae (CP), n.k huweza kuongeza hatari ya wewe kupata ugonjwa wa pumu,

hasa ikiwa ulipata maambukizi mapema maishani. Inaonekana kwamba maambukizi ya kwenye mapafu ya utotoni yanaweza kubadilisha mazingira ya vijiumbe vidogo kwenye mapafu, na kuyafanya kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata uvimbe na kupungua kwa njia ya hewa,hali inayosababishwa na pumu.

>>Soma hapa kuhusu Dalili za ugonjwa wa pumu.

8. Mtoto kuzaliwa mapema,kabla ya wakati,Mtoto njiti(Premature birth)

Mtoto Kuzaliwa kabla ya wakati kunaweza kusababisha mtoto kupata matatizo ya mapafu na kupumua, ikiwa ni pamoja na pumu.

Miili ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati haijakomaa vizuri, na ukuaji huu wa mapema unaweza kusababisha shida kwa watoto katika maisha yao yote hadi utu uzima.

Vichochezi vya Kupata Pumu(Triggers)

Kuwa kwenye Mazingira yenye vichochezi vya Pumu kuna uwezekano wa kusababisha dalili za pumu kwa watu walio na pumu. Wakati mwingine dalili hizi zinaweza kuwa kali. Vichochezi vya kawaida vya shambulio la pumu ni pamoja na:

  • Uchafuzi wa hewa(air pollution),mfano Uchafuzi wa hewa kutokana na moshi kutoka kwenye viwanda,magari,Moto wa nyika n.k
  • Tatizo la acid reflux
  • Hewa kuwa kavu na baridi
  • disinfectants na bidhaa nyingine za kusafisha
  • Baadhi ya Sabuni
  • Vumbi
  • Baadhi ya vyakula
  • Maambukizi ya Viruses kama ya Mafua n.k
  • Baadhi ya Dawa
  • Uvutaji wa Sigara n.k

#SOMA Zaidi hapa; Kuhusu ugonjwa wa pumu.

Rejea Link;

•https://www.healthline.com/health/asthma/is-asthma-contagious#what-causes-asthma

•https://afyaclass.com/2021/07/asthmacauses-risks-of-ashtma-symptoms_20.html

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa5 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...