Ticker

6/recent/ticker-posts

Madaktari waliokuwa wakiendelea na mgomo kusimamishwa kazi kenya



#Kenya: Chama cha madaktari na matabibu nchini Kenya, KMPDU kimesema kwamba “hakitalegeza msimamo wake” wala kuridhia kurejea kazini hadi pale hatima ya madaktari wanafunzi itakapojulikana.

Kufuatia kauli hizo, baraza la magavana linatishia kuwaachisha kazi madaktari wanaogoma kwani serikali za kaunti ndiye muajiri wao.

Mwenyekiti wa baraza la magavana, Anne Waiguru, alisisitiza kuwa daktari yeyote ambaye hatarejea kazini haraka iwezekanavyo atachukuliwa hatua za kisheria. Aidha ameongeza masuala waliyowasilisha madaktari yanaanza kufanyiwa kazi.



Post a Comment

0 Comments