Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanamtandao maarufu wa TikTok Nchini Iraq auawa kwa Risasi



Mwanamtandao maarufu wa TikTok Nchini Iraq auawa kwa Risasi

Mwanamtandao maarufu wa TikTok Nchini Iraq aitwaye Ghufran Sawadi maarufu kama Om Fahad, ameuawa kwa risasi nje ya nyumba yake mashariki mwa Mji Mkuu wa Baghdad Ijumaa usiku ambapo camera za usalama zilimnasa Muuaji aliyevalia mavazi meusi akishuka kwenye pikipiki na kumpiga risasi.

Tayari Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq imesema imeunda Timu ya Wataalamu kuchunguza mazingira ya mauaji ya Mwanamtandao huyo aliyekuwa na Wafuasi wanaokaribia nusu milioni pamoja na likes zaidi ya milioni tatu kwenye mtandao wake wa Tiktok ambao aliutumia kuweka video zake akicheza nyimbo mbalimbali, kutoa misaada kwa Watu na kuonesha maisha yake binafsi.

Februari mwaka 2023 Ghufran alihukumiwa kwenda Jela miezi sita kwa kosa ambalo Mahakama ilisema ni la kusambaza video za maongezi machafu ambayo yanadhoofisha adabu na maadili ya Jamii ya Nchi hiyo ambapo Watayarishaji wengine watano wa maudhui mtandaoni walihukumiwa jela hadi miaka miwili kwa makosa mbalimbali katika maudhui yao.

Hii ilikuja baada ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq mwezi January mwaka 2023 kuzindua Kamati ya kugundua maudhui machafu na yenye kudhalilisha ambayo yamekuwa yakiwekwa mitandaoni na Raia wa Nchi hiyo wenye ushawishi kama Om Fahad ambapo Serikali ilisema wanachokifanya ni kulinda maadili na mila za familia katika Jamii ya Wairaq.



Post a Comment

0 Comments