Ticker

6/recent/ticker-posts

Umri wa mtoto kuota meno pamoja na dalili zake,fahamu Zaidi hapa



Umri wa mtoto kuota meno pamoja na dalili zake,fahamu Zaidi hapa

Umri wa kuota meno ya kwanza kwa mtoto

Muda wa kuota meno kwa watoto hutofautiana kati ya mtoto mmoja na mwingine, baadhi ya watoto huzaliwa na meno ya awali na wengine huota meno baada ya miezi 4 hadi mwaka. Hata hivyo tegemea mwanao kupata meno akiwa ndani ya mwaka wake wa kwanza toka amezaliwa. Tafiti zinaonyesha watoto wengi huota meno yao ya kwanza wakiwa na miezi sita. Dalili zifuatazo zinaweza kuwa ishara ya mtoto kuota meno ya kwanza.

Dalili za meno kuota kwa mtoto

Maumivu ya fizi na kubadilika rangi (kuwa na rangi nyekundu wakati meno yanataka kutoka nje)

Shavu moja la mtoto hubadilika rangi

Mtoto huchokonoa masikio(kwa sababu ya miwasho au maumivu)

Kutoa udenda zaidi ya kawaida

Hupenda kutafuna na kusugua fizi zaidi ya kawaida

Mtoto kulialia na kusumbua isivyo kawaida

Kuweka mikono kinywani na kuinyonya

Kung’ata ziwa la mama anapokuwa ananyonya

Kupata homa kiasi

Kuharisha(hii ni baadhi ya dalili ambayo huripotiwa na wazazi)

Pitia makala ya dalili zinazoambatana na kuota meno kwa maelezo zaidi.

Kumbuka endapo mtoto akipata homa halisi yaani joto la mwili kupanda kiasi cha nyuzi joto za centigredi 38, wasiliana na daktari kwa sababu kuota meno huwa hakusababishi kupata hivi kwa joto.

Kwa sababu watoto wengi huota meno kwenye umri wa kuanzia miezi sita, ni vema mzazi ukawa na tabia ya kusafisha meno hayo, tumia mswaki wa watoto kusafisha meno ya mtoto kwa kutumia dawa ya meno yenye fluoride mara mbili kwa siku ili kuimarisha meno yake. Hakikisha mtoto hamezi dawa.

Pia katika kipindi hiki msaidie mtoto kuondoa maumivu ya jino kwa kutumia panado kulingana na dozi uliyoelekezwa na daktari wako. Kanda sehemu jino linapoota ili kuondoa maumivu na kumtuliza mtoto. Tumia vifaa maalumu pia kumwekea kinywani ili mtoto apate kung’ata na kujisikia vema dhidi ya miwasho ya meno kuota. Kuwa makini hata hivyo mtoto asimeze au kupaliwa.

Meno huota kwa mpangilio upi?

Maelezo ya hapa chini yameelezea wastani wa umri wa kuota meno kwa watoto walio wengi, hii ndio maana kuna utofauti wa maelezo haya na picha hapo juu. Ili kufahamu meno yanayozungumziwa ni yapi, tazama picha juu kufananisha.

Meno ya insiza ya chini kwanza

Huanza kuota kwenye umri wa miezi 5 hadi 7

Meno ya insiza ya juu

Huanza kuota kuanzia miezi 6 hadi 8

Meno ya insiza ya pembeni juu

Huanza kuota kuanzia miezi 9 hadi 11

Meno ya insiza ya pembeni chini ya taya

Huanza kuota kuanzia miezi 10 hadi 12

Meno ya kwanza ya mola

Huanza kuota kuanzia miezi 12 hadi 16

Meno ya kanaini

Huanza kuota kati ya miezi 16 hadi 20

Meno ya pili ya mola

Huanza kuota miezi 20 hadi 30

Kwa maelezo zaidi pitia picha hapo juu.

Ni umri gani meno yote ya kwanza huwa yameota?

Watoto wengi huwa wameshaota meno yao yote ya awali mpaka wanapfikia umri wa miaka 2 na nusu

Soma zaidi kuhusu makala zingine kwa kubofya makala zingine zinazohusu:

Chanjo kwa mtoto

Hatua za ukuaji wa mtoto

Namna ya kumfanya mtoto ale chakula zaidi

Namna ya kuandaa lishe ya mtoto

Namna ya kunyonyesha mtoto

Wakati gani maziwa ya mama huanzakutoka baada ya kujifungua?

Utapiamlo

Uandaaji wa lishe ya mtoto

Ukuaji wa mtoto wa kawaida(uzito na urefu

Maendeleo ya mtoto Mwaka 1 hadi 2

Maendeleo ya mtoto Miaka 2 hadi 3

Maendeleo ya mtoto Miaka 3 hadi 5



Post a Comment

0 Comments