Ticker

6/recent/ticker-posts

Usipime presha baada ya kunywa vinywaji kama vile Pombe, vinywaji venye Caffeine, Kahawa



Usifanye Mambo haya wakati wa Upimaji presha;

1. Usipime presha baada ya kunywa vinywaji kama vile Pombe, vinywaji venye Caffeine, Kahawa n.k

2. Usipime presha kama umevuta sigara dakika 30 zilizopita

3. Usipime presha kama ndyo umetoka kufanya mazoezi,kukimbia,kutembea n.k, pumzika kidogo kabla ya kuanza kupima presha

4. Wataalam wa afya hushauri hata kama ulikuwa hufanyi kazi yoyote,unashauriwa kutulia angalau kwa dakika 5-10 kabla ya kuanza kupima presha yako

5. Hakikisha unakaa vizuri kwenye kiti,huku miguu hujaikunja(maarufu kama kukunja Nne),kaa kawaida tu,huku ukinyoosha mkono wako ambao upo upande wa Moyo kwa ajili ya kuanza vipimo

8. Hakikisha miguu yako miwili imegusa chini au imekanyaga chini ya Floor wakati unapima presha

9. Usijifunge cuff ya kupimia presha juu ya shati,hakikisha mkono unakuwa wazi na kipimo kinagusa ngozi ya mwili wako

10. Pia hakikisha unafunga cuff kwenye Msuli wa mkono na sio chini ya kiwiko cha mkono au karibia na viganja vya mkono

11. Hakikisha mpira wa kipimo chako unaangalia kwa juu na sio nyuma ya mkono wako

12. Pia unashauriwa Usiongee wakati wa kupima presha yako



Post a Comment

0 Comments