Ticker

6/recent/ticker-posts

Kenya Mafuriko, shughuli za baharini zazuiwa tahadhari ya Kimbunga Hidaya



Kenya Mafuriko, shughuli za baharini zazuiwa tahadhari ya Kimbunga Hidaya

Wakazi wa kaunti ya Lamu hawataruhusiwa kusafiri baharini kuanzia leo jioni hadi siku ya Jumanne kufuatia tahadhari ya Kimbinga Hidaya.

Wavuvi na abiria wameshauriwa kukatiza safari zao.

Viongozi wa Lamu walikutana kujadili namna ya kuepuka maafa wakati Kimbunga Hidaya kikitarajiwa.

William Samoe, Kamanda wa Polisi eneo la Lamu ametoa wito kwa wakaazi kutii maagizo wanayopewa na kwamba suala hili litachukuliwa kwa uzito mkubwa.

Abiria kwa sasa wametakiwa kuvaa majaketi ya kuokoa maisha na pia kutopakia abiria wengi kupita kiasi kwasababu kwasasa bahari itakuwa inashuhudia mawimbi makali na mvua.

Chanzo: Bbc



Post a Comment

0 Comments