Ticker

6/recent/ticker-posts

Mfalme Charles akiwa kwenye Ziara yake ya kwanza ya umma tangu alipogunduliwa saratani



Mfalme Charles akiwa kwenye Ziara yake ya kwanza ya umma tangu alipogunduliwa saratani.

Mfalme Charles, ambaye alikuwa kwenye mapumziko katika majukumu ya kifalme ili kuzingatia afya yake, amerejea katika majukumu rasmi ya umma kwa mara ya kwanza tangu kugunduliwa na saratani.

Mfalme huyo mwenye umri wa miaka 75, alitembelea kituo cha matibabu ya saratani mjini London leo Aprili 30, ambapo alikutana na wataalam wa matibabu na wagonjwa wengine.

Charles, ambaye ni mlezi wa shirika la kusaidia saratani la Macmillan Cancer Support, alifika katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Macmillan Cancer Center katikati mwa London Jumanne asubuhi na mkewe, Malkia Camilla.

Ziara ya wawili hao inalenga kuangazia umuhimu wa utambuzi wa mapema na kuangazia utafiti wa kibunifu unaofanyika katika kituo cha matibabu.

Buckingham Palace pia ilitangaza Jumanne kwamba Mfalme ndiye mlinzi mpya wa kifalme wa Utafiti wa Saratani Uingereza.

Charles alionekana akipungia mkono umati mkubwa wa watu waliokusanyika nje ya kituo cha matibabu, na alisikika akifanya mzaha alipofika.



Post a Comment

0 Comments