Ticker

6/recent/ticker-posts

Mtu wa kwanza kupandikizwa Figo ya nguruwe afariki dunia



Boston, Massachusetts, USA

“Bw Slayman,Mwanamume wa kwanza kupandikizwa figo ya nguruwe iliyobadilishwa vinasaba amefariki miezi miwili baada ya upasuaji huo, hospitali iliyotekeleza utaratibu huo imesema.

Richard “Rick” Slayman, umri 62, alikuwa akiugua ugonjwa wa figo hatua ya mwisho kabla ya kufanyiwa upasuaji huo mnamo mwezi Machi.

“Rick alisema kuwa moja ya sababu zilizomfanya afanyiwe utaratibu huu ni kutoa matumaini kwa maelfu ya watu wanaohitaji upandikizaji kuishi,”

Hospitali kuu ya Massachusetts (MGH) ilisema Jumapili hakuna dalili kwamba kifo chake kilikuwa matokeo ya upandikizaji. Hospitali hiyo ilisema “imehuzunishwa sana” na kifo chake cha ghafla na kutoa rambirambi kwa familia yake.



Post a Comment

0 Comments