Connect with us

Magonjwa

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Avatar photo

Published

on

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni, ndani ya Afyaclass tulitoa elimu mbali mbali kuhusu Ugonjwa huu,

Na leo Katika Makala hii tunazidi kukuelimisha Uujue Vizuri Ugonjwa huu wa macho Mekundu Maarufu kama RED EYES.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu

Ugonjwa wa macho mekundu ni ugonjwa ambao hujulikana kama Red Eyes,

Ugonjwa wa red eyes ni ugonjwa ambao huhusisha macho kuwa mekundu kama dalili kubwa.

Katika Makala hii tumechambua chanzo cha Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes), dalili Zake kuu, jinsi ya kuzuia usipate Pamoja na Matibabu yake.

CHANZO CHA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

Ugonjwa wa Macho mekundu(Red Eyes) hutokana na mashambulizi ya vimelea vya magonjwa kama vile Virusi ambavyo husababisha vishipa vidogo ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

Maambukizi ya kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalam “Viral Keratoconjunctivitis” ni Maambukizi yanayosambaa kwa kasi kubwa .Hakuna tiba maalum kwa ugonjwa huu na hata bila tiba, dalili huisha zenyewe ndani ya wiki mbili . Usafi ni jambo muhimu katika kuzuia maambukizi haya kusambaa kwa wengine.

Mlipuko huu husababishwa na Kirusi kijulikanacho kwa jina la “Adenovirus”kwa zaidi ya asilimia 80%.

Dalili za Ugonjwa wa Macho Mekundu

DALILI ZA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NI PAMOJA NA;

• Macho kubadilika rangi na kuwa mekundu,

hii ni ishara ya Vishipa vidogo vya damu ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

• Kuwashwa na macho

• Kuhisi kitu kama mchanga ndani ya jicho lako

• Kuvimba macho yako

• Kuhisi hali ya kuungua ndani ya macho,

Hii ni ishara ya kutengeneza hali ya vidonda ndani ya jicho(Conjunctivitis Sore),

• Macho kuwasha au kutoa maji/nachozi yenyewe n.k

Ni nini cha Kufanya Kama Una Ugonjwa wa Macho Mekundu(Red Eyes)?

Ikiwa jicho lako haliumi na kuona kwako hakujaathiriwa, labda sio jambo kubwa. Ugonjwa huu wa macho mekundu(Red Eyes) unaweza kupona wenyewe ndani ya siku chache.

Mpaka Unapona Unashauriwa;

  • Kutokugusa au kusugua macho yako
  • Usivae miwani inayogusa macho, na kama kuna ulazima wa kuvaa,Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa
  • Zingatia Usafi

JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

– Watoto wadogo Wagonjwa wanaoenda shule wanashauriwa wakae nyumbani hadi dalili zinapoisha kwa kuwa ni ngumu kuzuia maambukizi yasisambae kwenye mazingira ya shule.

– Watu wazima wanaweza kwenda kazini ila wanapaswa kuzingatia kanuni za kuzuia kutokuambukizwa au kuambukiza wengine kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

– Watumishi wa Afya wazingatie kutopeleka Maambukizi hayo nyumbani kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

Zingatia Zaidi Mambo Haya Muhimu;

1. Usisugue au kupikicha macho yako,

Uchafu pamoja na Viini vya magonjwa(germs) kwenye mikono yako pamoja na Vidole vinaweza kusababisha hali Zaidi ya Wekundu na Muwasho ndani ya macho.

2. Kama unavaa miwani, Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa

3. Zingatia Usafi kwa Ujumla, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mikono yako unanawa kwa maji safi tiririka na Sabuni

4. Kwa Wale wanaopaka MakeUp, Hakikisha unaondoa MakeUp yako Vizuri na kuacha macho yako yakiwa Safi(Remove your eye makeup properly, and keep your eyes clean).

5. Pata Mapumziko ya mara kwa mara, ikiwa unafanya kazi zinazohusisha kuangalia computer screen kwa Muda Mrefu.

6. Epuka vitu ambavyo huweza kuleta usumbufu(irritation) wowote machoni kama vile; vumbi,moshi n.k

7. Hakikisha unaenda kuchunguzwa macho au kufanya Vipimo vya macho(Eye exam) ikiwa una shida ya macho kuwa mekundu mara kwa mara au Ikiwa hali ya macho kuwa mekundu haiishi.

MATIBABU YA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU(RED EYES)

– Ugonjwa huu wa Macho mekundu(red eyes) hupona wenyewe ndani ya siku 3 mpaka 5, ndani ya wiki 2 n.k kulingana na uwezo au uimara wa kinga yako ya mwili Wala huhitaji matumizi ya dawa yoyote ile.

Japo lazima kwanza kuchuguzwa na wataalam wa afya baada ya kujihakikishia kuwa ni shida ya red eyes watakupa maelekezo kwa kina ikiwa ni pamoja na jinsi ya kutunza jicho lako.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa4 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa7 hours ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa4 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa3 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending