Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapa



Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapa

Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapa.

malaria sugu

Malaria Sugu au Chronic malaria ni pale ambapo ugonjwa wa Malaria umekuwa wa muda mrefu ambapo kwa kitaalam tunasema ni "long-term malarial infection" 

Kumbuka: Tofauti ya Malaria Sugu(chronic Malaria) na malaria ya muda mfupi(acute Malaria) ni kwenye Swala la muda tu wa mashambulizi,madhara yake pamoja na matibabu yake,

ambapo Malaria Sugu ni tatizo la muda mrefu,lakini acute malaria;mgonjwa huugua malaria baada ya muda mfupi hupona kabsa na kurudi kwenye hali yake ya kawaida pasipo maambukizi tena.

Hivo basi,Malaria Sugu na Malaria yakawaida ya muda mfupi,vyote husababishwa na vilemelea sawa,dalili sawa n.k

CHANZO CHA UGONJWA WA MALARIA SUGU

Malaria Sugu ni ugonjwa ambao husababishwa na vimelea vya magonjwa viitwavyo Plasmodium, vimelea ambavyo huendelea kufanya mashambulizi kwa muda mrefu ndani ya mwili wako.

Vimelea hivi vya Plasmodium vinavyosababisha Malaria Sugu(chronic Malaria) vipo vya aina mbali mbali kama vile;

  • Plasmodium vivax,
  • plasmodium malariae,
  • plasmodium falciparum,
  • plasmodium ovale

Vimelea hivi huenezwa na mbu jike aina ya anofelesi (anopheles). Lakini watu wengi huelewa kwamba malaria husababishwa na mbu. Mbu huyu husaidia katika usambazaji tuu wa vimelea husika.

Dalili za Malaria Sugu

DALILI ZA MALARIA SUGU NI PAMOJA NA KUPATA DALILI HIZI MARA KWA MARA NDANI YA MUDA MREFU;

1. Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa

2. Mgonjwa kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika

3. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kichwa

4. Mgonjwa kuhisi hali ya kizunguzungu kikali

5. Hamu ya kula au appetite ya chakula kupotea

6. Wakati mwingine mgonjwa kutoa jasho sana

7. Mgonjwa kuwa na dalili zote za kuchanganyikiwa au kuweweseka sana wakati malaria ikiwa kali

•Soma zaidi hapa,Kuhusu dalili za ugonjwa wa Malaria

VIPIMO VYA MALARIA SUGU

Moja ya vipimo ambavyo hutumika kupima ugonjwa wa Malaria Sugu ni pamoja na kipimo cha Damu kwa kutumia kifaa kinachoitwa MRDT,hadubini n.k.

Malaria Sugu,endapo Ugonjwa wa Malaria haujatibiwa huweza kusababisha madhara zaidi mwilini ikiwemo;

  • Kusababisha tatizo la kuvimba kwa bandama,kwa kitaalam hujulikana kama hyper-reactive malarial splenomegaly (HMS),
  • Matatizo kama vile; Kuchanganyikiwa,
  • Na hata Mtu kupoteza Maisha kabsa.

MATIBABU YA UGONJWA WA MALARIA

Mgonjwa wa malaria hutibiwa baada ya kufanyiwa vipimo kwa kutumia dawa mbali mbali kama vile; ALU au mseto, Malaffin, Quinine N.K

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je, Malaria Sugu husababishwa na nini?

Malaria Sugu ni ugonjwa ambao husababishwa na vimelea vya magonjwa viitwavyo Plasmodium, vimelea ambavyo huendelea kufanya mashambulizi kwa muda mrefu ndani ya mwili wako.

Vimelea hivi vya Plasmodium vinavyosababisha Malaria Sugu(chronic Malaria) vipo vya aina mbali mbali kama vile;

  • Plasmodium vivax,
  • plasmodium malariae,
  • plasmodium falciparum,
  • plasmodium ovale

Vimelea hivi huenezwa na mbu jike aina ya anofelesi (anopheles). Lakini watu wengi huelewa kwamba malaria husababishwa na mbu. Mbu huyu husaidia katika usambazaji tuu wa vimelea husika.

Hitimisho

Ni muhimu sana kufahamu kuhusu dalili za Ugonjwa wa Malaria ikiwemo Malaria Sugu,ili kuhakikisha unafanya vipimo na kupata tiba mapema zaidi kabla ya kupata madhara zaidi,

DALILI ZA MALARIA SUGU NI PAMOJA NA KUPATA DALILI HIZI MARA KWA MARA NDANI YA MUDA MREFU;

1. Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa

2. Mgonjwa kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika

3. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kichwa

4. Mgonjwa kuhisi hali ya kizunguzungu kikali

5. Hamu ya kula au appetite ya chakula kupotea

6. Wakati mwingine mgonjwa kutoa jasho sana

7. Mgonjwa kuwa na dalili zote za kuchanganyikiwa au kuweweseka sana wakati malaria ikiwa kali

Ukiona dalili kama hizi,hakikisha unawahi hospitalini kwa ajili ya Vipimo pamoja na Matibabu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments