Uzazi/Ujauzito
LINI MAMA MJAMZITO(MAMA KIJACHO) AANZE KLINIKI?
LINI MAMA MJAMZITO(MAMA KIJACHO) AANZE KLINIKI?
KABLA hata mwanamke HAJABEMBA MIMBA,kama ana plan ya Kubeba MIMBA,Inashauriwa mwanamke na Mwenzi wake Wafike hospitali kwa ajili ya USHAURI na baadhi ya Uchunguzi, hivo ndyo kiafya Zaidi inashauriwa.
lakini pia mama huyu mara moja anaanzishiwa madini kwajili ya maandalizi ya mtoto, hapa ndipo matumizi ya Fefol au FOLIC ACID huanza ili kuzuia mtoto asije zaliwa na Matatizo kama vile;
- Tatizo la mgongo wazi,
- kichwa kikubwa n.k,
- Lakini pia Vidonge hivi husaidia damu ya Mama Kuongezeka Zaidi
lakini pia kwa wenye magonjwa kama Ukimwi,presha,Homa ya ini yaani Hepatitis unaangaliwa, mfano kama Viral load Ipo chini sio risk kwa kumuambukiza mtoto na mengineyo kama ushauri wa kijumla juu ya lifestyle.
LINI MAMA MJAMZITO(MAMA KIJACHO) AANZE KLINIKI?
Ingawa Protocol za Hospital na hospital huweza kutofautiana kwa habari ya Muda wa kuanza hudhurio la Kwanza la Kliniki kwa Ujauzito; ila Kwa ujumla,MAMA MJAMZITO Anashauriwa AANZE CLINIC MARA TU ANAVYOGUNDUA AMEPATA UJAUZITO au Aanze Hudhurio la kwanza la Ujauzito kabla ya kufikisha wiki 16 za ujauzito.
Mahudhurio ya Kliniki yamegawanyika katika makundi manne kulingana na Umri wa Ujauzito japo yanaweza kuzidi manne kulingana na Hali ya Ujauzito.
- Hudhurio la kwanza ni Ujauzito kabla ya kufika wiki 16
- Hudhurio la Pili ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 20-24
- Hudhurio la Tatu ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 28-32
- Na hudhurio la Nne ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 36-40
Nb; Mahudhurio haya yanaweza kuzidi manne kulingana na Hali ya Ujauzito,mfano mama akiwa na magonjwa mengine kama presha n.k
Chat Nasi Whatsapp
"Ungana na Wasomaji zaidi ya 12,000 wanaopata huduma ndani ya afyaclass,Kama unachangamoto yoyote ya kiafya;Kwa Ushauri&Tiba tuwasiliane hapa kupitia WhatSapp,Kama huna Whatsapp tuma SMS au Piga +255758286584."
Chat WhatSapp HapaNB: Ikiwa umegundua una MIMBA,Plan kuanza clinic mapema, Na unatakiwa kwenda na mwenzi wako hasa kwa ajili ya kupata Ushauri pamoja,Kufanya vipimo kama vile vya Ukimwi,Homa ya Ini(hepatitis),group za damu kama Hazipo tofauti.n.k
Mfano: Unakuta mwanamke HANA MAAMBUKIZI ya VVU,mwanaume ANAYO(Discordant couple),Tukipima na kujua hili,Mnazingatia ushauri ili Kumlinda mtoto (ndio FAIDA za kuja mapema).
lakin Pia kama WOTE wanamaambukizi Pia kuna ushauri Tunatoa,Lengo ni kumlinda mtoto asizaliwe na MAAMBUKIZI. kuna FAIDA nyingi sana za kuja kapata Uchunguzi mapema mkiwa wote Wawili.
UMUHIMU WA MAHUDHURIO YA KLINIKI KWA MAMA MJAMZITO
VITU VYA MUHIMU KATIKA MAHUDHURIO YOTE KWA UJUMLA WAKE
UMUHIMU WA MAHUDHURIO YA KLINIKI KWA MAMA MJAMZITO
- kutokwa na Damu ukiwa Mjamzito
- Kutokwa na uchafu wenye harufu kali ukeni hii ni dalili ya maambukizi kama Fangasi
- Miguu kuvimba kupita kiasi,mikono pamoja na Uso
- kuona Maruerue wakati wa Ujauzito
- kutokumsikia mtoto anacheza tumboni zaidi ya masaa 24 kwa mama ambaye umri wa mtoto kucheza tumboni umefika mfano kuanzia wiki 20-24. endelea kutufwatilia kujua zaidi…
- Presha kupanda na kuwa na Protein kwenye mkojo,hiki ni kiashiria kikubwa cha Ugonjwa wa Kifafa cha Mimba
VIDONGE VYA KUONGEZA DAMU
KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
Medical Disclaimer
Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.
Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?
💬 Wasiliana na Daktari Hapa

