Ticker

6/recent/ticker-posts

MAMBO YANAYOWEZA KUPELEKEA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE



 MAMBO YANAYOWEZA KUPELEKEA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE

Unaweza kushangaa kusikia nguvu za kike kwani sio maarufu sana kama swala la nguvu za kiume katika jamii zetu,ila hata kwa wanawake kuna nguvu za kike na ni muhimu pia kuzingatiwa,katika makala hii tumechambua baadhi ya sababu zinazochangia kuathiri nguvu za kike.

Katika suala zima la mapenzi kwa mwanamke yapo mambo mengi sana ambayo yanaweza kuadhiri afya na utimamu wa mfumo wa mapenzi wa mwanamke.mwanamke ili apate hisia,msisimko na mshindo katika mapenzi ni lazima kuwe na maelewano mazuri katika mfumo wa fisiolojia pamona na saikolojia yake.  Endapo saikolojia ya mwanamke haipo vizuri basi ni lazima apate upungufu wa nguvu za kike,kadhalika kama fisiolojia ikiwa haipo vizuri atapata upungufu wa nguvu za kike. Katika mfumo wa fisiolojia ya mwanamke kuna vichocheo ambavyo ni lazima vibalansi ndyo mwanamke anakua timamu kwenye suala la mapenzi,vichocheo hivyo ni Estrogen, progesterone na testosterone. Kadri umri wa mwanamke unavozidi kwenda kunatokea mabadiliko katika saikolojia na fisiolojia yake na hivo basi kua na upungufu wa nguvu za kike ama kupoteza kabisa hamasa ya tendo la ndoa

MAMBO YAFUATAYO HUPELEKEA MWANAMKE KUPATA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE

UMRI:Umri wa mwanamke unavozidi kwenda fisiolojia na saikolojia yake hubadilika sana na hivo huweza pia kuleta shida ya upungufu wa nguvu za kike.

UZAZI:Mwanamke anapokua katika na mimba au kunyonyesha. Saikolojia yake huipa kipaumbele mtoto sana,hivo hamasa na hamu ya kuwa na mwanaume hupungua sana

UZITO MKUBWA/KIRIBA TUMBO: Mwanamke anapokua na uzito mkubwa/kiribatumbo hupata mabadiliko makubwa ya vichocheo katika mwili wake vikiwemo vichocheo vya Estrogen, progesterone,luteinizing, FSH na testosterone. Mabadilko haya hupelekea mwanamke kupata upungufu wa nguvu za kike n.k.

KUNDI LA WANAWAKE AMBAO WAPO KWENYE HATARI YA KUPATWA NA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE NI PAMOJA NA;

Wanawake wenye kisukari na shinikizo la damu

Wanawake wenye matatizo ya dundumio

Wanawake wenye ugonjwa wa PCOS

Wanawake waliokeketwa

Wanawake wenye PID

Wanawakwe wenye historia ya kuachwa,kubakwa au kunyanyaswa kwa namna yeyote

Wanawake wenye matatizo ya kushika mimba

Wanawake wanaovuta sigara,bangi na kunywa pombe

Wanawake wanamichezo

Wanawake wenye uvimbe kwenye uke,kizazi au kwenye nyoga

Wanawake wenye tatizo la Msongo wa mawazo

Wanawake wenye ugonjwa wa endometriosisi na adenomaiyosis

Wanawake wenye tatizo la kujikojolea

Wanawake ambao wana maisha duni,kama kutokua na hela n.k

MAMBO MENGINE YANAYOCHANGIA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE

Kama nilivokwisha kusema hapo awali mwanaume anaweza kua chanzo cha upungufu wa nguvu za kike. Leo napenda niweke mkazo kwenye mambo manne yafuatayo

KUTWANGA UKE; wanaume wengi wamekua na kasumba ya kudhani kwamba ili waonekane vidume ni lazima awe na uume mkubwa na mreefu kama wa punda,ni lazima aingize uume kwa nguvu,lazima mwanamke akunjwe kunjwe vibaya. Ndugu zangu wanaume,katika sehemu ambayo mwanamke anapataga raha ni kwenye mdomo wa uke kwa juu kidogo,kaa theluthi moja ya urefu wa uke kwa juu kutoka nje.

Maeneo hayo ambayo ndio vitovu vya raha ni kinembe au kiarage na G SPOT. haya maeneo yakifanyiwa kazi vizuri ni lazima mwanamke aridhike na ajisikie vizuri tu. ndugu wanaume kule ndani ya uke unapokua unasukuma mpaka mwisho ni kwa manufaa ya mwanaume tu na sio kwa mwanamke. wanaume wengi wanadhani kutumia nguvu kusukuma ndani ndo uanaume au ndo utaonekenana unafanya kazi kubwa lakini kinyume chake huleta shida kubwa sana kwa wanawake.

Dhana ya kwamba utaonekana kidume kama mwanamke akitoka akiwa anachechemea ni ujinga,ulimbukeni na muendelezo wa mfumo dume kwenye mausuala ya mapenzi. Mwanamke ambae hajapata matumizi kwa maana amefurahia tendo,amefika kileleleni ni rahisi kufurahia kitendo hiki na hatakua na upungufu wa nguvu za kike.  Wanaume badilikeni na chezeni na maneo nloyataja hapa na kwenye post ya jana. Wanaume acheni kuiga vitendo kwenye video za ngono kwani wale wajamaa hawapo kufurahishana wapo kwenye biashara zao za hovyo na hivyo kuiga hapo na kutaka kuonyesha kwa mwanamke wako ni ushamba na kutaka kumletea matatizo ya kiafya na hasa katika suala zima la nguvu za kike

PUNYETO; kumekua na ongezeko la wanawake kupiga punyeto aidha kwa kutumia dildo,karoti,bamia,ndizi,pump za maji ya kutawazia vyooni nk. Upigaji huu wa punyeto umekua chanzo kikuu kingine cha upungufu wa nguvu za kike kwani saikolojia ya mapenzi hubadilika na kuhamia kwenye vitu hivo ambavyo si kutoka kwa binadamu. Wanawake acheni kupiga punyeto

MAPENZI YA KINYUME NA MAUMBILE: Hii pia ni changamoto kwa sasa kwani mwanamke akishazoea huko basi inabadilisha saikoljia yake
.KUSAGANA

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments