Ticker

6/recent/ticker-posts

Mapigo ya moyo kwenda mbio, chanzo, dalili, na Matibabu ya Tachycardia



 Mapigo ya moyo kwenda mbio, chanzo, dalili, na Matibabu ya Tachycardia

Tachycardia ni tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio ambapo huhusisha kiwango cha mapigo ya moyo kuwa zaidi ya mapigo 100 kwa dakika.

Tatizo hili la Mapigo ya moyo kwenda mbio linaweza kutokuwa na dalili au matatizo yoyote. Lakini likiachwa bila matibabu, baadhi ya aina za tachycardia zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya, ikiwa ni pamoja na tatizo la kushindwa kwa moyo kufanya kazi(heart failure), kiharusi au kifo cha ghafla.

Matibabu ya tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio yanaweza kujumuisha matumizi ya mbinu maalum, dawa, cardioversion, au upasuaji ili kudhibiti mapigo ya moyo yanayokwenda kwa kasi.

Dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Moyo ukienda kwa kasi sana, huenda usisikume damu ya kutosha kwenda kwenye sehemu nyingine za mwili. Kama matokeo, viungo na tishu zinaweza kutopata kiasi cha kutosha cha oksijeni.

Kwa ujumla, tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio linaweza kusababisha dalili na ishara zifuatazo:

  1. Kuhisi moyo kwenda kasi sana
  2. Kupata Maumivu ya kifua
  3. Kuzirai (syncope)
  4. Kupata Kizunguzungu
  5. Moyo kupiga kwa kasi sana
  6. Kupumua kwa shida n.k

Baadhi ya watu wenye tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) hawana dalili zozote. Hali hii inaweza kugundulika wakati wa uchunguzi wa mwili au vipimo vya moyo vinapofanywa kwa sababu ya tatizo lingine.

Chanzo cha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Tachycardia ni ongezeko la kasi ya mapigo ya moyo kwa sababu yoyote. Inaweza kuwa ongezeko la kawaida la mapigo ya moyo kutokana na mazoezi au majibu ya mkazo kwa kitaalam (sinus tachycardia). Sinus tachycardia inachukuliwa kuwa ni dalili, si ugonjwa.

Mambo yanayoweza kusababisha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio ni pamoja na:

  • Homa
  • Matumizi makubwa ya pombe au kuacha kutumia pombe ghafla
  • Kiwango kikubwa cha kafeini
  • Shinikizo la damu la juu au chini
  • Kutofanana kwa viowevu mwilini vinavyoitwa electrolytes - kama vile potasiamu, sodiamu, kalsiamu na magnesiamu
  • Madhara ya dawa
  • Tezi la Koo Kufanya kazi kwa kasi (hyperthyroidism)
  • Kupungua kwa kiasi cha chembe chembe nyekundu za damu (anemia), mara nyingi husababishwa na kutokwa na damu
  • Uvutaji wa sigara
  • Matumizi ya dawa za kulevyia/haramu, ikiwa ni pamoja na dawa zenye vichocheo kama vile kokaini au methamphetamine n.k

Jinsi ya Kuzuia tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Chukua hatua zifuatazo:

✓ Kula lishe bora. kitu unachokula huweza kuleta faida au madhara mwilini,hivo chagua mlo kamili wenye virutubisho vyote muhimu,

kula nafaka nzima, nyama isiyo na mafuta mengi, maziwa yasiyo na mafuta mengi, matunda, na mboga mboga za Majani. Punguza matumizi ya chumvi, sukari, pombe, mafuta mengi, na mafuta yenye utomvu(saturated fat and trans fats).

✓Fanya mazoezi mara kwa mara. Jaribu kufanya mazoezi angalau dakika 30 kila siku.

✓ Dhibiti Uzito wako wa Mwili. Kuwa na uzito uliozidi kunaweza kuongeza hatari ya kupata  magonjwa ya moyo pamoja na matatizo mengine kama vile tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio.

✓ Dhibiti shinikizo la damu na viwango vya cholesterol. Fanya mabadiliko ya mtindo wa maisha na tumia dawa kama ilivyopendekezwa ili kudhibiti shinikizo la juu la damu (hypertension) au viwango vya cholesterol vilivyopanda.

✓Acha kuvuta sigara. Ikiwa unavuta sigara na huwezi kuacha peke yako, ongea na mtoa huduma wako wa afya kuhusu mikakati au programu za kukusaidia kuacha tabia ya kuvuta sigara.

✓ Acha kabsa matumizi ya Pombe au Kunywa kwa kiasi. Ikiwa unachagua kunywa pombe, fanya hivyo kwa kiasi. Kwa watu wazima wenye afya, hiyo inamaanisha kunywa chupa moja ya pombe kwa siku kwa wanawake na chupa mbili kwa siku kwa wanaume.

Kwa baadhi ya hali za Kiafya, inashauriwa kabisa kuacha pombe. Uliza ushauri kutoka kwa mtoa huduma wako wa afya kuhusu hali yako maalum.

✓ Usitumie dawa za kulevyia au kichocheo, kama vile kokaini. Ongea na mtoa huduma wako wa afya kuhusu programu inayofaa kwako ikiwa unahitaji msaada wa kuacha matumizi ya dawa za kulevyia.

✓ Tumia dawa kwa uangalifu. Baadhi ya dawa za kukabili homa na kikohozi zina viyeyusho ambavyo vinaweza kusababisha mapigo ya moyo kwenda kwa kasi. Uliza mtoa huduma wako wa afya ni dawa gani unahitaji kuepuka.

✓ Punguza matumizi ya kafeini. Ikiwa unakunywa vinywaji vyenye kafeini, fanya hivyo kwa kiasi.

✓ Dhibiti msongo wa mawazo. Tafuta njia za kupunguza msongo wa Mawazo, Kufanya mazoezi zaidi ikiwemo kufanya mazoezi yanayohusisha utulivu wa akili n.k ni baadhi ya njia za kupunguza msongo wa mawazo.

✓ Fanya chekups mara kwa mara. Pata uchunguzi wa mwili mara kwa mara na ripoti mabadiliko yoyote katika mapigo yako ya moyo kwa mtoa huduma wako wa afya. Ikiwa dalili zako zinabadilika au kuwa mbaya au unapata dalili mpya, mwambie mtoa huduma wako wa afya mara moja.

✓ Usijaribu kujitibu mwenyewe. Ikiwa una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) au wasiwasi kuhusu afya yako ya moyo, usijaribu kujitibu mwenyewe. Ni muhimu kumuona mtoa huduma wa afya kwa uchunguzi na ushauri sahihi.

✓ Tafuta matibabu mapema. Ikiwa una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) au dalili zingine ambazo huzielewi tafuta matibabu mapema. Kupata utambuzi na matibabu sahihi kwa wakati kunaweza kusaidia kuzuia matatizo makubwa zaidi ya kiafya.

✓ Elewa historia yako ya Kiafya. Jifunze kuhusu historia yako ya Kiafya na historia ya magonjwa ya moyo katika familia yako. Hii itasaidia daktari wako kutambua hatari kwako ya kuwa na  tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) pamoja na matatizo mengine ya moyo.

✓ Epuka sababu zinazoweza kusababisha tachycardia. Kama ilivyoelezwa hapo juu, kuna sababu kadhaa zinazoweza kusababisha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio. Kwa kuzingatia mtindo bora wa maisha na kufuata miongozo ya kuzuia magonjwa inaweza kupunguza hatari kwako ya kuwa na tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia).

Kumbuka, Ikiwa una wasiwasi kuhusu afya yako au una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio, tafadhali wasiliana na mtoa huduma wako wa afya kwa ushauri na matibabu sahihi. Kujali afya yako ni muhimu ili kuishi maisha yenye afya na furaha.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments