Ticker

6/recent/ticker-posts

Mpox ni nini? Mpox/Homa ya Nyani



Mpox ni nini? Mpox/Homa ya Nyani

Kumekua na mlipuko barani Africa, nchi za jirani pia zimetangaza kua na wagonjwa wa mpox. Hivi karibuni hata mabara mengine yameanza kutangaza uwepo wa ugonjwa huu kwa kasi, hiii imepelekea WHO kuutangaza ugonjwa wa homa ya nyani kama janga la kimataifa. Hata hivyo nchini Tanzania bado hakujatangazwa kupatikana kesi ya ugonjwa huu.

Homa ya nyani ni ugonjwa unaosababishwa na virusi.virusi hivi ni familia moja na virusi vinavyosababisha smallpox au ndui kwa kiswahili.

Tuone historia ya Homa ya nyani kifupi.

Homa ya nyani sio ugonjwa mpya, umegundulika mwaka 1958 katika nyani waliokua wakifanyiwa tafiti. Kesi ya kwanza ya homa ya nyani kwa binadamu iligundulika mwaka 1970 nchini  DRC.

Tangu wakati huo kumekua na kesi chache barani africa hasa  africa ya kati na afrika ya magharibi. Lakini mwaka 2022 tumeanza kuona ugonjwa huu ukienea kwa kasi maeneo ambayo sio endemic na hata nje ya bara la Africa.

Unaambukizwaje

  1. Mji maji au mate yanatotoka kinywani wakati wa Kuongea, kukohoa au kuoiga chafya. (Droplets)
  2. Aina zote za ngono zinaweza kuambukiza, hii inajuimuisha kumbusu mtu mwenye mpox(All forms of sexual contact including kissing)
  3. Kukutana au kugusana ngozi na mtu mwenye homa ya nyani (Skin to skin contact)
  4. Kuvaa nguo au kutumia mashuka na foronya za mtu mwenye homa ya nyani. (Sharing clothes and/or bedding)
  5. KUgusa au kula wanya walioathirika au mizoga.

Dalili

  1. Upele (una wezakutokea kwenye ngozi, mdomoni, ukeni, au ndani ya njia ya haja kubwa)
  2. Homa
  3. KUskia maumivu kwenye koo. (Sore throat)
  4. Maumivu Kichwa
  5. Maumivu ya Misuli
  6. Maumivu ya mgongo
  7. Uchovu wa kupitiliza usio elezeka
  8. Kuvimba tezi

Tiba na chanjo

  1. Homa ya nyani isiokua na dalili kali (severe) hupona yenyewe ndani ya wiki 2-4 ( self limiting)
  2. Nenda kituo cha afya kuhakiki kama ni mpox na sio kitu kingine.
  3. Matibabu ya upele na kutibu dalili zingine kama homa kali na maumivu ya misuli yanaweza kupatikana

Chanjo ya homa nyani ipo lakini bado haipatikani nchi nyingi za Africa.

Watu walio katika hatari Ya kupata Homa ya nyani yenye Dalili Kali (severe).

  1. Watoto chini ya mwaka mmoja
  2. Wajawazito
  3. Watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

Watu walio katika hatari ya kupata homa ya nyani

  1. Watoa huduma ya afya
  2. Wanaofanya kazi katika mkusanyiko/msongamano  wa watu wengi
  3. Watu wenye wenza wengi ( multiple sexual partners)
  4. Watu wenye kujihusisha na biashara ya ngono
  5. Wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja pia wametajwa kuwa na hatari ya kupata.

Jinsi ya kujikinga

  1. Epuka sehemu zenye msongamano  ambazo utagusana na watu
  2. Nawa mikono kabla ya kujigusa, kula, au unapotoka kwenye mizunguko
  3. Tumia kinga wakati wa kujamiiana
  4. Epuka kugusa wanyama wanaumwa au mizoga bila kujua ugonjwa au sababu ya kifo.

Jinsi ya kuwalinda wengine endapo wewe umeathirika.

  1. Kaa nyumbani au katika chumba chako mwenyewe kama inawezekana.
  2. Osha mikono mara nyingi kwa sabuni na maji au na vitakasa mikono, hasa kabla au baada ya kugusa vidonda.
  3. Vaa barakoa na funika vidonda unapokuwa karibu na watu wengine hadi upele wako upone.
  4. Weka ngozi yako kavu na bila kufunikwa (isipokuwa unapokuwa chumbani na mtu mwingine).
  5. Epuka kugusa vitu katika maeneo ya pamoja na safisha maeneo ya pamoja mara kwa mara.
  6. Fuata maelekezo ya daktari katika kutibu vipele/vidonda.
  7. Tumia dawa za kupunguza maumivu zinazopatikana bila agizo la daktari kama vile paracetamol au ibuprofen.

 Nini cha kuepuka

Kupasua au kukuna vipele/malengelenge. Hii inaweza kuweka vijidudu kwenye vidonda na kusababisha vishambuliwe na bakteria au kuchelewa kupona kwa vidoonda. Au kusambaza zaidi mwilili.

Kwa Taarifa, msaada na ushauri zaidi piga simu namba 199

Credits|Article By;sms sharing button

Dr Ladina Msigwa

Dr Ladina Msigwa



Post a Comment

0 Comments