Connect with us

Others

Ndugulile achaguliwa Mkurugezi Mkuu WHO Afrika

Doctor Ombeni

Published

on

Imeboreshwa July 27, 2026 by Doctor Ombeni

Ndugulile achaguliwa Mkurugezi Mkuu WHO Afrika

CONGO, Brazzaville – Mbunge wa Kigamboni na Naibu Waziri wa Afya wa zamani Dk Faustine Ndugulile ameshinda uchaguzi wa kiti cha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Dunia Kanda ya Afrika.

Katika Uchaguzi uliofanyika leo jijini Brazzaville nchini Congo, wajumbe 25 kati ya 46 wa Mkutano Mkuu wa 74 wa WHO uliofanyika leo wamemchagua Ndugulile na hivyo kuwashinda wagombea wengine kutoka Niger na Senegali.

Tayari Ndugulile ameweka wazi kuwa vipaumbele vyake ni kuhakikisha Watu wanapata haki ya kupata huduma bora za afya, Kuboresha utayari wa nchi za Afrika katika kukabiliana na majanga ya magonjwa ya mlipuko, Kuimarisha uwajibikaji ndani ya WHO kanda ya Afrika pamoja kuimarisha mawasiliano baina ya nchi wanachama katika masuala ya Afya.

🏆Certified| Doctor from Afyaclass.Hapa utapata Ushauri & Tiba juu ya magonjwa mbali mbali. Kwa msaada Zaidi Tuwasiliane kupitia namba: +255758286584.Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *