Ticker

6/recent/ticker-posts

Wagonjwa 171 wamekutwa na homa ya nyani,Mpox Burundi



Wagonjwa 171 wamekutwa na homa ya nyani,Mpox Burundi

Wizara ya afya nchini Burundi imesema wagonjwa 171 wamekutwa na homa ya nyani.

Tangazo hilo linafuatia kisa cha kwanza cha ugonjwa huo kuthibitishwa nchini humo mwezi uliopita.

Waziri wa afya Polycarpe Ndayikeza ameliambia shirika la habari la AFP kuwa, hadi sasa hakuna vifo vyovyote vilivyoripotiwa kutokana na ugonjwa huo.

Mwishoni mwa mwezi Julai, wagonjwa watatu walikutwa na mpox nchini Burundi huku wizara ya afya ikithibitisha wagonjwa wengine 153 waliokutwa na virusi vya homa ya mnamo mnamo Agosti 18.

Wizara hiyo imetahadharisha kuwa ugonjwa wa mpox unaendelea kuenea kwa kasi na kwamba imeanzisha mchakato wa kuweka wodi maalum katika hospitali za wilaya ili kushughulikia wagonjwa wa homa ya nyani.

Afisa mmoja wa afya ameliambia shirika la habari la AFP kuwa, wagonjwa waliokutwa na homa ya nyani wanashukiwa kuwa na aina mpya ya kirusi cha mpox kinachosambaa kwa kasi katika nchi Jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Via:DW.



Post a Comment

0 Comments