Connect with us

CHANJO

WHO yataka uwekezaji zaidi kwenye chanjo ya kipindupindu

Doctor Ombeni

Published

on

Imeboreshwa July 28, 2026 by Doctor Ombeni

WHO yataka uwekezaji zaidi kwenye chanjo ya kipindupindu

Mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO ametoa wito wa kuongezwa uzalishaji wa chanjo ya kipindupindu, akiangazia kile alichokielezea kuwa upungufu mkubwa kabisa wa chanjo hiyo uliwenguni.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kupitia ukurasa wa X kwamba, visa 307,433 vya kipindupindu na vifo 2,326 vimeripotiwa katika mataifa 26 hadi Julai 28, ingawa udhibiti wake unazidi kuathiriwa na upungufu mkubwa wa chanjo.

Nchi 18 zimeagiza dozi milioni 105 tangu mwezi Januari, lakini ni dozi milioni 55 tu zilizotengenezwa.

Ghebreyesus amehimiza uwekezaji zaidi utakaosaidia kuongeza uzalishaji wa chanjo lakini pia kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na usafi kwa ujumla ili kuzuia milipuko zaidi ya kipindupindu.

🏆Certified| Doctor from Afyaclass.Hapa utapata Ushauri & Tiba juu ya magonjwa mbali mbali. Kwa msaada Zaidi Tuwasiliane kupitia namba: +255758286584.Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *