Ticker

6/recent/ticker-posts

Afariki akifanyiwa Upasuaji wa Kuongeza Makalio



Afariki akifanyiwa Upasuaji wa Kuongeza Makalio

Mama wa Watoto watano aitwae Alice Delsie Preete Webb (33), amefariki dunia baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio Nchini Uingereza ikielezwa kuwa alifanyiwa upasuaji huo na Mtu asiyekuwa na mafunzo rasmi ya kitiba.

Maafisa wa Polisi wameanzisha uchunguzi juu ya kifo chake na tayari Watu wawili wamekamatwa na kuachiliwa kwa dhamana wakikabiliwa na tuhuma za mauaji ya Alice ambapo imeandika kuwa huduma hiyo hugharimu pound 2,500 ( zaidi ya milioni 9 Tsh. ) na hufanyika ndani ya dakika 60 tu.

Alice ambaye anatajwa kuwa Muingereza wa kwanza kufariki kutokana na upasuaji wa aina hiyo, ameacha Mume na Watoto wao watano ambao ni Delsie (15), Preete (13), Gracie (12), Nylie (10) na Clarie (7).



Post a Comment

0 Comments