Ticker

6/recent/ticker-posts

Chanzo cha Sikio kutoa Usaha au Maji Maji



 Chanzo cha Sikio kutoa Usaha au Maji Maji

• • • • • •

TATIZO LA KUTOKA USAHA AU MAJIMAJI MASIKIONI (OTORRHEA) chanzo chake

Tatizo la kutokwa na usaha au maji maji sikioni ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Otorrhea ni tatizo ambalo huweza kumpata mtu yoyote bila kujali umri wake wala jinsia yake.

Shida hii huweza kuanzia sehemu ya ndani ya sikio yaani Inner Ear, sehemu ya katikati ya sikio yaani Middle Ear na hata sehemu ya Nje ya sikio yaani Outer Ear.

DALILI ZA TATIZO HILI

- Mtu mwenye shida hii kwanza kabsa utaonekana usaha ndani ya sikio au maji maji yakitoka ndani ya sikio

- Sikio kuanza kutosikia vizuri au kuziba

- Wengine hupata maumivu ndani ya sikio

CHANZO CHA TATIZO LA KUTOKWA NA USAHA AU MAJI MAJI SIKIONI

Zipo baadhi ya Sababu mbali mbali ambazo huchangia uwepo wa tatizo hili la kutokwa na usaha au maji maji sikioni, na sababu hizo ni kama vile;

- Kupatwa na shida ya maambukizi ya Fangasi za masikioni ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Otomycosis

- Kupatwa na maambukizi ya Ugonjwa wa Tuberculosis(TB) ndani ya sikio

- Pia Mgonjwa wa Virusi vya ukimwi huweza kupatwa na shida hii ya kutokwa na usaha au maji maji masikioni

- Kupata tatizo la Kansa ya sikio ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Neoplasm

- Maambukizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa kama vile bacteria N.K ambayo huathiri ngoma ya sikio,sehemu ya katikati ya sikio pamoja na sehemu ya Nje ya sikio lako

- Kuchomwa na kitu chochote chenye ncha kali sikioni au Kuingiwa na kitu chochote sikioni kama vile; punje ya mahindi,maharage,mdudu, Kijiwe N.K

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments